Zinazobamba

KIFO CHA IMAMU SALUM ,VIONGOZI WA DINI YA KIISLAM WALIANGUKIA BUNGE LA JAMHURI WA MUUNGANO,WASEMA JESHI LA POLISI LAHUSIKA NA KIFO HICHO,SOMA HAPO KUJUA

NA KAROLI VINSENT
WAKATI  Familia ya  Marehemu Imamu salum Alhamis wakiwa wameugomea kuuzika wa Mwili marehemu  huyo  mpaka pale Jeshi la polisi litakapokubali kuhusika na kifo hicho.
Nao Shuira ya Maimamu nchini wameibuka na kulitaka bunge la Jamhuri ya Muungani nchini kuunda tume ya kuchunguza tukio la kifo cha marehemu Salum kwa madai kifo chake kimegubikwa na utata mkubwa.
Wamesema Maelezo ya yaliyotolewa na Kamishna wa kanda maalum ya Polisi Dar es Salaam,Saimon Sirro kuwa Imani Salum aliuliwa na Polisi kwa sababu ya kutaka  kuiba fedha  zilizokuwa  zimefikishwa kwenye mashine ya kutolea fedha ATM maeneo ya kurasini Jijini Dar es Salaam hayaendani na maelezo ya wazazi wa marehemu si ya kweli.
Akizungumza na waandishi wa habari leo  Kiongozi wa Shuira ya Mamimu nchini,Sheikh Yusuf Muhamed amesema baada ya kubaini maelezo haya ya polisi juu ya kifo hicho hayana ukweli ndio sababu ya kulitaka bunge lichunguze ili kuondokana na matatizo yanayotokea.
“Tunaliomba Bunge liunde kamati lichunge tukio hili,na tume hii itakayowahusisha  wataalamu na viongozi wa kada mbali mbali,ili ichunguze kwa kina mauaji makubwa yanayoshamiri dhidi ya raia na viongozi wa hapa nchini,”
“Ichunguzi mauaji hayo ni yale yanayifanywa  na kikundi kisichoeleweka nay ale yanayofanywa na chombo rasmi cha Dola Jeshi la Polisi”amesema  Sheikh Muhamedi