Zinazobamba

Mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi februari mwaka 2017 umeongezeka


vlcsnap-2017-03-08-17h28m03s471
Ofisi ya taifa ya Takwimu (NBS) imesema  mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi  februari  mwaka 2017 umeongezeka hadi kufika  asilimia 5.5 kutoka asilimia 5.2 mwezi januari 2017.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam,kaimu meneja wa  idara ya takwimu za ajira na bei kutoka ofisi ya taifa ya Takwimu(NBS) Bi.Ruth Minja amesema   kuwa kasi ya upandaji wa bei imeongezeka ukilinganisha na mwaka uliyoishia mwezi januari2017
Amebainisha kuwa farihisi za bei zimeongezeka hadi 106.97 mwezi februari 2017 kutoka 101.44 mwezi ambapo mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi  umeongezeka hadi asilimia 8.7 kutoka asilimia 7.6 kwa mwezi januari 2017.
Ametaja  baadhi ya vyakula vilivochangia kuongezeka kwa farihisi ni pamoja na mchele kwa asilimia 4.0 mahindi kwa asilimia 12.2,unga wa mahindi kwa asilimia 10.1,mtama kwa asilimia 5.6,ndizi za kupika kwa asilimia 9.5 na maharage kwa asilimia 6.7
Bi.Minja amesema kuwa  ongezeko la mfumuko  wa bei kwa nchi ya Tanzania ni mdogo ukilinganisha na nchi nyingine za afrika mashariki Kenya na Uganda.
Kaimu meneja wa idara ya takwimu za ajira na bei  Bi.MINJA ameongeza kuwa  mfumuko wa bei  wa nchi ya kenya ni asilimia 9.04 kutoka asilimia 6.99 na upande wa Uganda mfumuko wa bei   umeongezeka kutoka asilimia 6.7 kutoka asilimia 5.9