Zinazobamba

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAAKE DUNIANI: WANAWAKE WAIPONGEZA SERIKALI

   Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mwanamke Duniani Bi. Devotha Likokola akizungumza na hadhira. Likokola amepongeza mashirika yote kwa kuweza kuungana na kufanikisha siku hiyo muhimu kwa wanawake.


 NA MWANDISHI WETU
 Imeelezwa kuwa katika kuhakikisha dhamira ya serikali ya awamu ya tano ya kufanya Tanzania kuwa Nchi ya viwanda,Wanawake wanapaswa kupewa kipaumbele ili kutimiza dira hiyo kwani wao ni msingi wa mabadiliko ya Kiuchumi na kwamba wako tayari kuibeba ajenda hiyo na kuifanya Tanzania kuwa Nchi ya viwanda.

Sambamba na hilo, Wanawake wameipongeza Serikali kwa jitihada zao wanazozifanya za kumlinda Mwanamke ikiwemo maboresho ya sheria, sera, na mikakati mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ambayo imelenga kumuinua mwanamke Kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Hayo yameelezwa na Mashirika yanayotetea haki za binadamu na wanawake wakati wakiazimisha siku ya Wanawake duniani inayofanyika kila March 8 ya mwaka husika.
 
Akitoa tamko kwa niaba ya mashirika hayo Bi.Naemy Silayo amesema kuwa siku hii huadhimishwa duniani kote kwa lengo la kutambua na kupongeza juhudi mbalimbali  za kumkomboa mwanamke kijamii,kisiasa na kiuchumi ambapo nchi zote duniani huitumia siku hiyo kufanya tathmini ya hali za wanawake na kuzitaka jamii husika pamoja na serikali kuendelea   kutetea wanawake na kuhamasisha ulinzi wa haki za wanawake.

Ametaja baadhi ya changamoto wazokumbana nazo wanawake ni pamoja na ubaguzi wa kijinsia,kunyimwa fursa za elimu,sharia kandamizi,uwepo wa mila na tamaduni kandamizi,mfumo dume,ukatili majumbani ikiwemo rushwa ya ngono wanawake kukatazwa kufanya kazi na kunyimwa haki ya kumiliki mali za familia pamoja na kuzuiwa kurithi mali.

Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha sheria na Haki za Binadamu Bi. Hellen Kijo Bisimba akizungumza maadhimisho ya siku ya mwanamke yaliyofanyika Jana Jijini Daresalaam.


Mwenyekiti wa chama cha ACT WAZALENDO Mama Anna Mgwira akisikiliza kwa makini Hotuba mbalimbali katika maadhimisho hayo ambayo na yeye alishiriki kama mmoja kati ya wanawake waliodhubutu na kuweza kugombea nafasi kubwa ya Urais nchini akiwa ni mwanamke pekee kufanya hivyo katika uchaguzi Uliopita

Naemy Silayo akitoa Tamko la wanawake katika Shughuli hiyo.


Mwanasheria Rebeca Gyumi (Mwenye kipaza sauti) akifafanua jambo katika mkutano huo, Gyumi amesema ipo haja ya kuangaliwa kwa baadhi ya sharia kandamizi na kutoa mfano wa sharia ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo inaruhusu mtoto wa kike kuolewa katika umri wa miaka 15 au 14 jambo ambalo ni la kikatili na linalomnyima fursa mtoto wa kike kuendelea na masomo pamoja na sheria za kimila ya mwaka 1963 inayoathiri fursa ya wanawake kiuchumi.

Rais wa Vikoba,Devotha Likokola ambaye alikuwa Mgeni Rasmi ambapo amesema kuwa Wanawake wanatakiwa kuzitumia fursa zilizopo katika sekta mbalimbali zitakazowasaidia kuondokana na utegemezi ili kuifikia Tanzania ya Viwanda