MBUNGE ZITTO KABWE AWAKASIRIKIA POLISI,NI KWENYE TUKIO LA WANAFUNZI KUANDAMANA,SOMA HAPO KUJUA
Kupitia Ukurasa wake wa Facebook kiongozi huyo ameandika hivi..
"Nawapongeza Sana Wanafunzi wa Bariadi walioandamana kudai haki yao ya
Mwalimu Mkuu wao kurejeshwa shuleni hapo. Jeshi la Polisi lilipaswa
kutoa ulinzi kwa Wanafunzi hawa na sio kuwapiga kama wahalifu. Wezi kama
kina Harbinder Singh Seth wa PAP/IPTL wanapewa ulinzi wa polisi na
usalama wa Taifa wakati watoto wanaodai haki ya Mwalimu bora wanapigwa.
OCD wa Bariadi na RPC wa Simiyu wawajibishwe kwa kutumia nguvu kubwa dhidi ya Wanafunzi hawa.
Nawashawishi Mtandao wa Wanafunzi Tanzania ( TSNP ) kuhamasisha
Wanafunzi nchi nzima waandamane kulaani wanafunzi wenzao kupigwa na
polisi huko Bariadi mkoani Simiyu"