Zinazobamba

MBUNGE ZITTO KABWE AWAKASIRIKIA POLISI,NI KWENYE TUKIO LA WANAFUNZI KUANDAMANA,SOMA HAPO KUJUA


Kupitia Ukurasa wake wa Facebook kiongozi huyo ameandika hivi..
"Nawapongeza Sana Wanafunzi wa Bariadi walioandamana kudai haki yao ya Mwalimu Mkuu wao kurejeshwa shuleni hapo. Jeshi la Polisi lilipaswa kutoa ulinzi kwa Wanafunzi hawa na sio kuwapiga kama wahalifu. Wezi kama kina Harbinder Singh Seth wa PAP/IPTL wanapewa ulinzi wa polisi na usalama wa Taifa wakati watoto wanaodai haki ya Mwalimu bora wanapigwa. 

OCD wa Bariadi na RPC wa Simiyu wawajibishwe kwa kutumia nguvu kubwa dhidi ya Wanafunzi hawa.

Nawashawishi Mtandao wa Wanafunzi Tanzania ( TSNP ) kuhamasisha Wanafunzi nchi nzima waandamane kulaani wanafunzi wenzao kupigwa na polisi huko Bariadi mkoani Simiyu"