ZITTO KABWE ASEMA HAYA,BAADA YA MBUNGE LEMA KUSHINDA RUFAA ZAKE MBILI ZILIZOFUNGULIWA NA SERIKALI,SOMA HAPO KUJUA
Baada ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania iliyokaa Arusha kutupa Rufaa
zote mbili zilizofunguliwa na Serikali dhidi ya maamuzi ya Mahakama Kuu
Kanda ya Arusha kuhusiana na dhamana ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless
Lema, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amezungumza.
Kiongozi huyo wa ACT ametumia Facebook kutoa malalamiko yake:
Mnamkamata mtu kwa kosa lenye dhamana. Mahakama Kuu inaruhusu dhamana. Serikali inakataa rufaa kuzuia dhamana. Mtu anakaa jela miezi 4, tena mwakilishi wa watu. Siku ya hukumu kuhusu dhamana Serikali inaondoa shauri mbele ya jopo la majaji 3. Lengo? Kumkomoa mtu. Siasa za ukomoaji zinajenga chuki kwenye jamii na chuki inazaa visasi. Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP. Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi.
Kiongozi huyo wa ACT ametumia Facebook kutoa malalamiko yake:
Mnamkamata mtu kwa kosa lenye dhamana. Mahakama Kuu inaruhusu dhamana. Serikali inakataa rufaa kuzuia dhamana. Mtu anakaa jela miezi 4, tena mwakilishi wa watu. Siku ya hukumu kuhusu dhamana Serikali inaondoa shauri mbele ya jopo la majaji 3. Lengo? Kumkomoa mtu. Siasa za ukomoaji zinajenga chuki kwenye jamii na chuki inazaa visasi. Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP. Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi.