TUNDU LISSU AIBWAGA TENA SERIKALI MAHAKAMANI,ACHIWA HURU,SOMA HAPO KUJUA

Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu imeitupilia mbali hati ya kiapo ya mkuu wa upelelezi Ilala, Mrakibu Msaidizi wa Polisi,
Denis Mujumba na kumuachia Tundu lissu
kwa dhamana.
Lissu yuko nje kwa dhamana ya shilingi milioni ishirini na mdhamini mmoja.
Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa mashtaka kumsomea Lissu ambaye ni Mbunge na mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani, mashtaka yake na kuwasilisha hati ya kiapo kupinga mbunge huyo kupewa dhamana.
Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo alisema kuwa kiapo kilichowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka kina mapungufu makubwa sana.
Amesema kuwa kukosekana kwa namba ya kesi na mahali ambapo inaonyesha muapaji wa kiapo hicho aliapa ni mapungufu makubwa.
Ameongeza kuwa mshtakiwa Lissu anahaki ya kupata dhamana kwa kuwa shtaka analokabiliwa nalo linadhaminika licha ya kuwa na kesi tatu tofauti mahakamani hapo kama ambapo kiapo kilivyosema.
Amesema kuwa, licha ya kuwa Lissu kweli Hana mashtaka mahakamani hapo lakini hakuna shtaka hata moja ambalo amekutwa na hatia na alilokutwa nalo na hatia
Kabla ya kiapo hicho jopo la mawakili wanne likiongozwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Mutalemwa Kishenyi aliyekuwa akisaidiana na Wakili Easter Martin, Jackline Nyantori na Clementina Masawe walimsomea
mshtakiwa mashtaka yake manne yanayomkabili ya kutoa lugha ya uchochezi.
Lissu ambaye amefikishwa katika viwanja vya mahakama hiyo leo majira ya
saa 11.42 asubuhi akiwa ndani ya land lover
ya polisi pamoja na msanii maarufu wa
uigizaji nchini Wema Sepetu na watuhumiwa wengine alikamatwa juzi mara baada ya kutoka kwenye viwanja vya
Bunge mjini Dodoma.
Lissu yuko nje kwa dhamana ya shilingi milioni ishirini na mdhamini mmoja.
Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa mashtaka kumsomea Lissu ambaye ni Mbunge na mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani, mashtaka yake na kuwasilisha hati ya kiapo kupinga mbunge huyo kupewa dhamana.
Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo alisema kuwa kiapo kilichowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka kina mapungufu makubwa sana.
Amesema kuwa kukosekana kwa namba ya kesi na mahali ambapo inaonyesha muapaji wa kiapo hicho aliapa ni mapungufu makubwa.
Ameongeza kuwa mshtakiwa Lissu anahaki ya kupata dhamana kwa kuwa shtaka analokabiliwa nalo linadhaminika licha ya kuwa na kesi tatu tofauti mahakamani hapo kama ambapo kiapo kilivyosema.
Amesema kuwa, licha ya kuwa Lissu kweli Hana mashtaka mahakamani hapo lakini hakuna shtaka hata moja ambalo amekutwa na hatia na alilokutwa nalo na hatia
Kabla ya kiapo hicho jopo la mawakili wanne likiongozwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Mutalemwa Kishenyi aliyekuwa akisaidiana na Wakili Easter Martin, Jackline Nyantori na Clementina Masawe walimsomea
mshtakiwa mashtaka yake manne yanayomkabili ya kutoa lugha ya uchochezi.
Saa
12:24 mchana, Lissu alipandishwa kizimbani Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, Wakili wa Serikali Mwandamizi,
Mutalemwa Kishenyi alidai kuwa mshtakiwa
huyo anakabiliwa na makosa manne ya kutoa lugha ya
uchochezi.
uchochezi.