Zinazobamba

NEMC YAWASIHI WATANZANIA AMBAO WANAOTAKA KUFANYA UWEKEZAJI,SOMA HAPO KUJUA

BARAZA laTaifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limewasihi wananchi  ambao wanataka kufanya shughuri za uwekezaji za miradi mbali mbali ,wanatakiwa kuwasiliana  na baraza hilo ili kufanyike tasmini ya athari ya mazingira kabla ya kuanza uwekezaji ili kuweza kuondokana na changomoto ya mazingira zinatazojitokeza.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa uenezi wa elimu ya mazingira ya (NEMC),Dkt Vedast Makota wakati akizungumza na Baadhi ya waandishi wa habari waliomtembelea ofisi za Baraza hilo kutaka kujua kazi za baraza hilo.

Ambapo Dkt Makota alitumia nafasi hiyo kuwasihi wananchi wanaotaka kuwekeza kwenye miradi mbali mbali ikiwemo Viwanda,Shule,Kumbi mbali mbali za starehe kuhakikiwa wanawasiliana na baraza hilo ili waweze kufanya tasmini ya athiri za mazingira.
“Kwa sasa tunapenda kuwasihi wawe wanawasiliana na sisi kabla hawajanza uwekezaji,kwa sasa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuharibu mazingira kunakosababishwa na uwezezaji usiofuta taratibu”amesema Dokta Makota.

Amesema kwa sasa endapo wananchi wakifanya tasmini ya athari ya mazingira kabla hawajawezekeza itasaidia katika kuondokana na matatizo ya mazingira.