Zinazobamba

BENKI YA DCB IMEENDELEA NA DROO YAKE,SOMA HAPO KUJUA


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Steven Dede akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na droo ya pili inatochezwa na benki hiyo ya weka amana na DCB na Boresha maisha na DCB


BENKI ya DCB imeendelea kufanya droo ya pili ya bahati nasibu ya pili ya kampeni ya kuweka Amani inayoitwa Boresha maisha na DCB huku Mkaguzi wa michezo ya kubahatisha (Bahati nasibu) Taifa Bakari Maggid na kufurahishwa kwa juhudi zinazofanywa na benki hiyo katika kuwapata washindi.

Droo hiyo iliyoanza mwezi Januari iliweza kuwapata washindi wa wa kwanza 20 waliopata tisheti, watatu waliopata fedha taslimu na wawili wakiopata simu za mkononi

Akizungumza kabla ya kuanza kwa droo hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa DCB Steven Dede amesema kampeni hiyo ilianza Novemba 28,2016 na droo hii ya pili ni kwa wateja walioekwa pesa kwenye akaunti zao kuanzia Desemba 28 hadi Januari 31.

Dede amesema akaunti zitakazohusika ni akaunti ya akiba binafsi, akaunti ya watoto na akaunti ya WAHI na kuwataka wateja wa benki hiyo na wasio wateja , watu binafsi, wajasirimalina taasisi mbalimbali kunendelea kujitokeza kwa wingi kushiriki shindano hilo kwa kufungua akaunti na kuweka amana.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa DCB akibonyeza kitufe kuashiria kuanza kwa droo hiyo akishuhudiwa na mkaguzi wa michezo ya kubahatisha( bahati nasibu) Taifa Bakari Maggid (wa pili kulia).