Zinazobamba

DC HAPI AKASIRIKIA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO KUOZEA BENKI,SOMA HAPO KUJUA

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi akikagua miradi mbali mbali kwenye Kata zilizopo kwenye Wilaya yake,ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi mbali mbali ya maendelea na kusikiliza kero za wananchi
NA KAROLI VINSENT
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi ameitaka manispaa hiyo,kuwasiliana na ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mtaa (TAMISEMI) ili watoe kibari cha kubadilisha matumizi hela milioni zaidi ya miliono 100  zilizokuwa zimetengwa kufanyia ukarabati  soko la mpunguni  ili zipelekwe kwenye soko la mandasi katika wilaya hiyo.
Hapi ametoa maagizo hayo leo wakati alipokuwa kwenye ziara katika kata ya Hananasifu ikiwa mwendelezo wa ziara yake ya siku 10 katika kata zote zilizopo kwenye Wilaya yake kwa lengo la kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.
Amesema amesikitishwa na hatua ya kata hiyo kushindwa kutumia milioni 100  zilizotengwa kwa ajili ya soko mpanguni kutokana na mgogoro.
"Yaani mmenishangaza sana fedha hizi  zimetengwa Tangu mwaka 2014 Mmeshindwa kuzitumia na kukaa Benki,kisa mgogoro huku ambao hauna mwisho,naitaka manispaa ya kinondoni iwasiliana na tamisemi ibadilishe matumizi ya fedha" amesema Hapi.
Amesema hawezi kukubali fedha hizo kukaa kwenye Benki bila kutumika huku zikipungua kutokana na makato ya Benki huku wananchi wakikosa maendeleo kutokana na migogoro isiyokuwa na Mwisho.
Katika hatua nyingeni Hapi,ameendelea na ziara yake katika kata ya Hananasisi na kufanikiwa kugagua masoko ,shule na baadae kuongea na wananchi wa kata hiyo ili kusikiliza kero za wananchi.