ZITTO KABWE AWASHUKIA WABUNGE WALEMAVU,SOMA HAPO KUJUA
KIONGOZI mkuu wa Chama cha ACT-wazalendo,Zitto Kabwe
amewashukia wabunge wa walemavu walioko ndani ya Bunge la Jamhuri wa Muungano
wa Tanzania kwa kusema wanavitetea vyama vyao vya siasa kuriko kuwatetea watu
wenye matatizo ya Ulemavu ambao wanakumbana na changamoto lukuki, Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo.
Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini ameyasema hayo
leo Jijini Dar es Salaam wakati ufunguzi wa wiki ya watu wenye ulemavu wa
kusikia,amesema Wabunge hao wamejikita kutetea vyama vyao na kushindwa kuweka
mbele maslai ya walemavu kwa kuwapambania matatizo yao.
“Yaani walemavu mnamatizo mengi sana,nashangaa sana
wa Wabunge wenye ulemavu ambao wapo ndani ya Bunge,wapo zaidi kuvitetea vyama
vyao,badala ya kuwatetea watu wenye ulemavu,huku wakijua watu wenye ulemavu
wanachangamoto nyingi sana,”amesema Zitto/
Zitto ambaye pia katika maisha yake alilelewa na
Mzazi wenye Ulemavu amewataka Wabunge wenzake kuhakikisha wanajitokeza katika
kuwasaidia watu wenye ulemavu katika nyanya mbali mbali.
Ametaja Nyanja hizo,ni kuwahakikisha wanasaidia
katika kupata masoko katika bidhaa zinazozalishwa na walemavu pamoja na
kuhakikisha wanahakikisha wanawekewa mazingira mazuri katika usafirishaji.