Zinazobamba

TNGP WATAJA MAFANIKIO YA URAGHBISHI NGAZI YA JAMII



Mkurugenzi Mtendaji wa Tgnp Mtandao Bi. Lilian Liundi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu mafanikio yaliyopatikana kufuatia kufanyika kwa utafiti wa uraghbishi katika wilaya saba za Ilala,Kisarawe, Kinondoni, Morogoro, Tarime na Mbeya.
Sehemu ya Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini.
 Wito umetolewa kwa jamii kuitumia dhana ya  utafiti wa uragabishi ili kuweza kuistua jamii kujitambua na kukua kimaendeleo 

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Mtandao wa Tgnp,Bi. Lilian Liundi wakati akitoa mafanikio yaliyopatikana kutokana na Mtandao huo kufanya utafiti wa namna hiyo.

 Liundi amesema utafiti wa Uraghabishi umesaidia kuleta mwamko katika Wilaya Saba ambazo wamezifanyia utafiti, kwani watu wengi wameweza kuchokozeka na kuanza kuhoji haki zao za msingi na hivyo kuongeza maendeleo katika kata zao.
 
Amesema katika utafiti wao walioufanya, katika wilaya za  Kisarawe, Kinondoni, Ilala, Morogoro, Tarime na Mbeya wameweza kufikia vikundi 222 , wanaume 1000 na wanawake 3000 na kugundua kuwa baada ya kufanya uragabishi kumekuwa na mabadiliko makubwa ya Kimaendeleo.
Aidha Kwa upande wake  afisa mipango, uchambuzi na machapisho  wa TGNP Bw. Deogratius Temba ameelezea dhana ya bajeti yenye mrengo wa kijinsia kuwa ni bajeti yenye macho yanayogusa makundi yote ya Kibinadamu.
Alisema kama kuna dhana kuwa bajeti yenye mrengo wa kijinsia ni kutaka kuwapendelea wanawaake inapaswa kuondoka kwani si tafsiri sahihi ya bajeti hiyo
Akizungumzia Tafsiri sahihi ya bajeti hiyo, Temba alisema ni bajeti yenye uhalisia ambayo itazingatia mahitaji ya kimakundi na hatimaye kitaifa.



Add caption