Zinazobamba

TAASISI ZA SERIKALI ZAPUUZA AGIZO LA MAGUFULI,NI KUHUSU WATUMISHI HEWA,SOMA HAPO KUJUA




NA KAROLI VINSENT
TAASISI  145  kati ya 409 za Serikali zimekaidi agizo la Rais John Magufuli lilowataka wawe wamewaondoa watumishi hewa, baada ya taasisi hizo kushindwa kuwasilisha  idadi ya watumishi wake serikalini ili watumishi hewa waweze gundulika.

Kutokana na hilo serikali imesema ifikapo tarehe 26 Agoust mwaka huu taasisi hizo ziwe zimewasilisha taarifa hizo,endapo zikiendelea kukaidi basi taasisi hizo zitawasilishwa kwa Rais Magufuli ili aweze kuzichukulia hatua.

Hata hivyo pia,taasisi 264 kati ya 409 za serikali ndio zimewasilisha taarifa za watumishi wake serikalini ambapo kati ya taasisi hizo 64 tu ndio zimethibitika hazina watumishi hewa huku taasisi 201 zimethibitika zinawatumishi hewa.

Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Angellah Kairuki wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema taasisi hizo zimekaidi agizo la Rais alilotoa tarehe 26 Mei 2016 ambalo alisema waajili wote wa taasisi hizo wawe wasilisha taarifa za mwisho za zoezi la kuwabaini na kuwaondoa watumishi hewa katika orodha za malipo ya mishahara.
Amesema Agizo hilo liliwataka waajili wote kuwsilisha taarifa iliyotajwa kuzingatia muundo wa uaandaji wa taarifa hizo serikali lakini amedai baadhi ya waajili wameshindwa kuwasilisha taarifa hizo.
“Tumewakumbusha sana waajili wawe wamewasilisha taarifa hizo ndani ya wiki mbili kabla ya tarehe  26 Agoust mwaka huu,endapo watashindwa kuwasilisha ili tuweze kuwajua watumishi hewa,sisi tutakachokifanya tutawasilisha kwa majini taasisi hizo kwa Rais Magufuli ‘Amesema Kiruki.
Hata hivyo Amesema ofisi yake imefanya jitihada mbali mbali za kuwaelimisha waajili mbali mbali ili waweze kuwabaini watumishi hewa pamoja na kuwazibiti.
Amedai mpaka sasa serikali imeshawaondoa watumishi hewa 16123 ambao walikuwa wanaitia hasara serikali ya Bilioni 16.5 kwa mwezi kwa malipo ya fedha,
Amesema kwa sasa amewaagiza watendaji wote kuwachukulia hatua  za kinidhamu pamoja na za kisheria kwa watendaji wote waliohusika kuwepo kwa watumishi hewa ili hatu zichukuliwe.