Zinazobamba

CHADEMA YAAENDELEA KUTESEKA,MADIWANI WAKE WAENDELEA KUKAMWATWA,SOMA HAPO KUJUA



Madiwani watatu wa Chadema na mfuasi mmoja wa chama hicho wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Rombo kwa makosa ya kufanya uchochezi. 

Madiwani hao, Nicolaus Kimario (Kirio), Anasia Kimario (Viti Maalumu), Daud Tarimo (Leto ) na mfuasi wa Chadema, Rogath Kanje walikana mashtaka hayo. 

Mwendesha mashtaka, Bernard Machivya alieleza mahakama kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Agosti 25, wakiwa nyumbani kwa mmoja wa washtakiwa Nicolaus Kimario. 


Aliieleza Mahakama kuwa washtakiwa wote wanne walitenda kosa hilo kwa pamoja wakifanya vikao vya kuhamasisha wananchi wajitokeze kwenye maandamano ya Ukuta Septemba Mosi. 

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Rombo, Naomi Mwerinde aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 5 na watuhumiwa wote wataendelea kukaa rumande.