Zinazobamba

SAKATA LA KUFUNGIWA DK MWAKA,LAZIDI KUCHUKUA SURA MPYA,SHIVYATIATA WAIBUKA NA KUSEMA HAYA,SOMA HAPO



Tabibu Juma Mwaka (Dk. Mwaka) wa kriniki ya Foreplan
Pichani ni Dk Mwaka



SIKU chache kupita baada Wizara ya Afya,Maendeleo  ya jamii,Jinsia wazee na Watoto,kupitia Baraza la tiba asili kuvifutia usajili wa kituo cha Fore plan  cha Dk Juma Mwaka na vingine viwili. kwa kile wanachodai vituo hivyo vikiuka kanuni ya Tiba asili.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Nalo Shirikisho la  Vyama vya tiba asili  nchini(SHIVYATIATA) limesema linakusudia kwenda mahakamani kutaka tafsiri ya   sheria ya tiba asili ya  namba 23 ya mwaka 2002  ambayo imetoa mwongozo wa tiba hizo.



Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa (SHIVYATIA)Abdulrahaman Lutenga amesema hawakubaliani na hatua ya Dr Edmund Kayombo ambaye ni mwenyekiti  ni Baraza la Tiba asili, jambo linalowasukuma  kwenda mahakamani ila mahakama itoe tafsiri ya sheria ili haki itendeke kwani hatua ya kufungiwa kwa taasisi hizo kumejaa siasa,
 Lutenga amesema hatua Dr Kayombo ya kuvifuta usajili  vituo vya tiba asili  huku vengine kufungiwa kwa miezi sita  hatua hiyo imekiuka sheria 23 ya mwaka 2002 ambayo inataka hatua  ifuatwe.

Amefafanua vifungu hivyo kuwa kuwa Uamuzi unaweza kutolewa na Baraza na bila ya kuwa na kikao cha kuwapelekea wajumbe nakala za shauri linalotakiwa kutolewa uamuzi wa kutoa maoni  yao kwa maandishi, 

Lakini pia amesema mjumbe  yeyote  anaweza kutaka uamuzi uhahirishwe na suala hilo lijadiliwe katika kikao cha baraza  lakini changushangaza kifungu hiko mwenyekiti huyo hakuzifuhata.
Amesema sanjari na hiyo pia hata maamuzi hayo hayakuzingatia taratibu na sheria  namba 23 ya tiba asili na mbadala ya mwaka 2002 sura ya nne kifungu cha 23 ukrasa wa 28.
"Amekiuka sheria ,na hata ukiangalia  maamuzi yake hayakuzingatia misingi na miiko ya tiba asili iliyojikita katika mila,desturi na utamaduni wa kitanzania yenye makabila zaidi 123”amesema Lutenga.
 Amesema hatua ya Baraza hilo kuvifungia vituo hivyo vitaleta athari kubwa kwa jamii kwani vilikuwa vimetoa ajira ya watanzania zaidi ya 3000 huku pia zikiwaponya watanzania masikini wanaotumia tiba hizo.
“Leo vituo vilivyokuwa na wafanyakazi zaidi ya 3000 leo unavifungia tena kwa kurupuka unategemea hawa watu wataishi vipi,harafu tena ukiangalia watanzania wanaotumia tiba za asili ni zaidi alimia 80 ya watanzania, leo unafungia vituo hawa watanzania masikini na wanyonge watapa tiba wapi,tunamuomba Rais Magufuli alitazame hili”amesema Lutenge.
Hata hivyo,Lutenga amesema licha ya baraza hilo kuchukua hatua hiyo amezidi ziomba Mamlaka husika kuwaondoa wafanyakazi kwenye baraza hilo kwani hawana dhamira ya kuendeleza tiba asili na tiba mbadala.
Aidha,Baraza hilo limemwomba Waziri wa Ummya Mwalimu kuwangalia kwa makini watendaji  baraza hilo kwani wamekuwa wakigongana.