Zinazobamba

PIGO TENA--HOTELI KUBWA ZAANZA KUPUNGUZA WAFANYAKAZI WAKE,BAJETI YA JPM YATAJWA,TRA WASEMA HAKUNA JINSI,SOMA HAPO KUJUA



Pichani ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,John Magufuli.


MACHANGU ya Bajeti ya  mwaka 2016/2017  yameaza kujionesha kwa kasi baada Hoteli kubwa  nchini ambazo zilikuwa zinatumika kuwapokea watalii kuanza kupunguza wafanyakazi katika hoteli hizo kwa kile wanachodai ukata wa fedha umezikumba Hoteli.(Mtandao huu umelezwa).Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Taarifa za kuamika ambazo Fullhabari.blog imezipata kutoka kwenye Hoteli moja maarufu jijini Dar es Salaam ambayo nayo imewaandikia baadhi ya wafanyakazi wake ikiwataka warudi nyumbani kwa kile wanachodai Hoteli hiyo inajiendesha kihasara.
 
Taarifa hiyo inasema kinachotwajwa kupelekea mpaka hoteli hiyo kuwa katika hali hiyo inatokana na hutua ya serikali kukataza mikutano yote ya serikali kufanyika kwenye Hoteli hizo huku ikitoa maelekezo kuwa mikutano yote ifanyike kwenye kumbi za serikali jambo ambalo linolotajwa kuliangamiza hoteli hizo  kwa kuwa  mikutano hiyo ni chanzo cha mapato.

Mbali na hilo pia kingine kinachotajwa kupelekea hasara ni hatua ya serikali pia kuongeza kodi ya watalii ambao wanaingia nchini jambo lilopelekea watalii kadhaa kusitisha safari zao kuja nchini.

Akizungumzia kwa sharti ya kutotaja jina lake meneja wa Hoteli moja ya kitalii iliyopo jijini Dar es Salaam amesema kwa sasa wamelazimika kuwapunguza wafanyakazi kwenye hoteli hizo ili waweze kuziokoa biashara zao.

‘Ninachokwambia ndugu  ni kweli tunapunguza wafanyakazi wetu maana hatuwezi tukawa na wafanyakazi wengi huku hakuna tunachokipata,wewe mwenyewe mwandishi unajau vyanzo vyetu vyote vya mapato vimekatwa na Bunge sasa unategemea sisi tuafanyaje,ndio maana tumeamua kufanya hivyo.”amesema  
“Yaani sahivi tunapika vyakula vinaishia kuchacha kwenye majokofu tu,maana wateja wetu ni watalii wa nje na sahivi umeshuhudia  kodi mpya ilivyowakimbiza watalii,ninachokwambi hakuna jinsi hakuna jinsi acha tujifunge mkanda kwa kupunguza wafanyakazi tu”ameeleza Bosi huyo.
  TRA WANENA.
Akizungumzia Kodi hiyo ya Watalii,Mkurugenzi wa Elimu na Huduma ya Mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato nchini (TRA),Emmanuel Kayombo amesema hakuna jinsi kodi hiyo lazima ikatwe ili nchi iweze kupiga hatua.
“Kodi ndiyo msingi wa kuliendeleza taifa,hata hao watalii wanaopinga kodi hiyo wamesahau kuwa kodi wanayolipa ndio itachangia kujengwa barabara  pindi wanapokuja kutalii,kwahiyo watanzania waelewe kodi hii itawaletea maendeleo”amesema Kayombo.
  WAZIRI DK MPANGO AFUNGUKA.
Akizungumzia  jana mkoani Mgorogoro wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wakaguzi wa ndani,Waziri wa Fedha na Mipango Dk Philipi Mpango amesema lengo la serikali kuhamisha mikutano toka kwenye Hoteli za Binafsi hadi kwenye Kumbi za wizara lengo ni kubana bajeti ili pesa itakayookolewa ielekezwe kwenye mipango ya Maendeleo.
Dk Mpango amesema hata sita kuakata mishahara watumishi wa serikali ambao watakaidi agizo hilo.