Zinazobamba

MSANII NISHA AONYESHA UPENDO WAKE KWA WATOTO MASIKINI,AFANYA JAMBO LA KUIGWA,SOMA HAPO KUJUA



nishaPichani ni Msanii Nisha akizungumza na Waandishi habari juu ya Futari aliyowaandalia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu Picha kwahisani ya Mtembezi.com.

nisha watoto
 Pichani ni watu mbali mbali wakijumuika wakati kupata futari iliyoaandaliwa na msanii huyo
Msanii wa Filamu mahiri ya “Kiboko Kabisa’ Salma Jabu maarufu kama (Nisha) amekuwa miongoni mwa watu mashuhuri waliojitolea kuwafuturisha watoto waishio katika mazingira magumu huku wengine wakitokea kituo cha Watoto Yatima cha New Hope Family kilichopo Kibada Mwasonga Dar es Salaam ambacho yeye ni msimamizi.

Watoto hao ambao walihudhuria mualiko wa futari viwanja vya shule ya Azania jijini Dar es Salaam walifikia hatua ya kumtoa machozi msanii huyo kutokana na dua mbalimbali walizokuwa wakisoma kuonekana kumgusa msanii huyo, ambapo amewataka wadau mbalimbali kuunga mkono jitihadfa hizo na ziwe endelevu ili kuwasaidia watoto hao kwani wanahitaji msaada wa karibu zaidi kama watu wengine.

Kwa upande wa watoto hao wametoa pongezi kwa Nisha huku wakimuombea Dua aendelee kuwaunga mkono kwa hali na mali, pia futari hiyo ilihudhuriwa na watu wengi mashuhuri akiwemo Eshe Buheti msanii wa Filamu, Jackline Wolper, Jini Kabula, Halima Yahya, Frola Mvungi, Snura Mushi, JK Comedian Rajai Ayoub  mshindi wa kwanza wamashindano ya Qur-an Afrika na wasita kidunia na wengine wengi.



Hakuna maoni