Zinazobamba

YAMETIMA SASA,MGODI WA BUZWAGI KUFUNGWA RASMI,YALIOSEMWA NA WABUNGE WA UPINZANI YATIMIA,SOMA HAPO KUJUA

Malori yakibeba mchanga wa dhahabu katika mgodi wa Buzwagi

MGODI wa Dhahabu wa Buzwagi uliopo Wilaya ya Kahama, Shinyanga unatarajiwa kusitisha shughuli za uchimbaji (Mining) na kuendelea na uzalishaji wa maeneo ya akiba yaliyoachwa awali kutokana na mmiliki wake kuishiwa. Anaandika Moses Mseti, Kahama … (endelea).
Mgodi huo unaomilikiwa na kampuni ya uchimbaji wa madini nchini ya Acacia, unatarajiwa kusitisha shughuli za uchimbaji (mining) ifikapo Juni mwaka huu kutokana na mmiliki wa mgodi huo kuishiwa fedha za kuendesha shughuli za uchimbaji.
Akizungumza jana katika ziara ya kushtukiza iliyofanywa mgodini hapo na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais (Muungano na Mazingira), Luhaga Mpina, Meneja wa Mgodi huo, Asa Mwaipopo, amesema gharama za kuendesha mgodi hazipo hivyo wanatarajia kutafuta mwekezaji mwingine atakaendelea na shughuli ya uchimbaji.
Amesema kuwa ifikapo Juni mwaka huu shughuli za kuendelea na uchimbaji (Mining) katika mgodi huo wa Buzwagi zitasimama na badala yake wataendela na uzalishaji wa maeneo ya akiba hadi mwaka 2019 watakapofunga rasmi shughuli za uzalishaji.
“Hatutafunga kabisa mgodi huu ambacho tutafanya ni kusitisha shughuli za uchimbaji (mining) kuanzia Juni, lakini ile akiba ambayo tulikuwa hatujaigusa tutaendelea nayo mpaka 2019 na kuufunga moja kwa moja na kama kuna mwekezaji mwingine atauziwa aendelee na uzalishaji,” amesema Mwaipopo.
Hata hivyo amesema sababu zilizopelekea mmiliki wa mgodi huo kuacha kuendelea na uchimbaji ni kutokana na kiasi cha fedha kilichotumika katika uwekezaji kuwa kikubwa ikilinganishwa na kibachozalishwa pamoja na gharama za kuendesha mgodi kupanda.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais (Muungano na Mazingira), Luhaga Mpina, amesema kuwa mwekezaji huyo amekomba dhahabu yote katika eneo hilo na kuondoka nayo, hivyo hasara haitakuwa kwa mwekezaji huyo bali itakuwa ni Taifa la Tanzania.
“Mmeondoa dhahabu yote alafu mnasema mnafunga mgodi hii ni hasara kwa Taifa na sio kwenu, mimi nafahamu kabla ya kuwekeza lazima utafiti wa wataalamu wenu ufanyike, hapa hakuna kufunga mgodi wala nini,” amesema Mpina.
Mbunge wa Kahama, Jumanne Kishimba, amesema kuwa licha ya mgodi huo kudai kwamba unaendesha shughuli zake kwa hasara lakini tatizo kubwa ni matumizi makubwa ya fedha kwa watumishi wa mgodi huo wanaofanya kazi Kahama na kuishi Dar es salaam.
“Kuna wafanyakazi wamegeuka miungu mtu katika mgodi huu, mtu anafanya kazi hapa Kahama analala Dar es Salaam, anatumia usafiri wa ndege kuja kazini unazani kuna faida watakayoipata kweli hawa,” amesema Kishimba.
 Habari hii kwahisani ya Mwanahalisi oline

Hakuna maoni