Zinazobamba

WAZIRI KAILUKI AUANGUKIA MFUKO WA RAIS KUHUSU TATIZO LA AJIRA KWA WAHITIMU WA CHUO KIKUU,SOMA HAPO KUJUA

Waziri Kairuki aitaka TAKUKURU kufanya kazi kwa bidii, kufuatilia rushwa ndogo na kuwa mfano kwa uadilifu


WAZIRI wa  nchi ofisi ya Rais ,Menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora,Angella Kairuki  amewataka watendaji wa mfuko wa Rais wa kujitegemea (PTF)  kuangalia uwezekano wa kuwawezesha wanafunzi wanaomaliza chuo kikuu ili waachane na fikra za kutegemea kuajiliwa badala yake wawe na  fikra za kujiajiri.Anaadika KAROLI VINSENT endelea nayo.
   Waziri Kailuki amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati alipofanya ziara kwenye ofisi za mfuko huo,ambapo amesema nia ya serikali ya kuanzisha mfuko huo ni kuwawezesha wananchi,lakini amewataka kuacha kuwaangalia peke yao wanafunzi wanohitimua katika vyuo vya ufundi pekee yao kama wanavyofanya sasa.
 “Kwa sasa kumekuwa na wanafunzi wengi wanaomaliza chuo kikuu wanakuwa hawana ajira huku fikra zao zinategemea kuajiriwa cha msingi hapa ni kuacha kuwafikilia wanaomaliza vyuo vya ufundi sahivi ni kuweka mkazo kwenye vyuo vikuu ili tuweze kuwaokoa na dhana ya kuajiriwa”amesema Waziri Kailuki.
Waziri Kailuki amesema kwa sasa mfuko huo kasi yake iliyotegemewa wakati inaanzishwa kwenye miaka ya 1984 kwa lengo la kuwawezesha wanatanzania waweze kujikwamua na hali ngumu ya maisha kutokana na viongozi wa mfuko huo kukosa utawala bora jambo aliloitaka bodi hiyo mpaka kufikia tarehe 5 ya mwezi ujao wawe wamepelekea sera ya ufanyaji kazi,
Ambapo amedai sera hiyo ikishaaandaliwa itapelekea kupunguza tatizo la  urasimu kwa wananchi wanapotaka huduma.
Awali akimkaribishwa Waziri, Mkuregenzi wa mfuko huo,Haigath Kitala amesema mfuko huo umeshindwa kufikia malengo yake ya kuwawezesha wajasiliamali kwa asilimia kubwa kutokana na kuelemewa na madeni jambo analodai limechangia mfuko huo kuwa nyuma.
Amedai kuwa licha ya kuwa na madeni hayo,pia hata Bajeti inayotengwa na serikali imekuwa ndogo ambayo hawezi kukidhi uendeshaji wa mfuko huo,sanjari na kukosa watumishi wa idara mbali mbali katika mfuko huo,
Akizungumia Changomoto hizo,Waziri Kailuki amewakikishia watendaji wa  mfuko huo kuwa atazifanyia kazi changomoto zao ili mfuko huo uondekane na tatizo hilo.  

Hakuna maoni