Zinazobamba

NI MUNGU TU NDIYE ATAKAYE MUOKOA ZITTO KABWE KWENYE KUPEWA CHEO CHA PAC,SAKATA LA ESCROW KUMPONZA,SOMA HAPO KUJUA

Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto 

MBUNGE wa Kigoma Mjini kupitia chama cha ACT-Wazalendo,Zitto Kabwe,jina lake limeondolewa kwenye nafasi ya uwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC).(Mtandao umedokezwa).Aaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
     Kabwe  ambaye alidumu kwenye nafasi ya hiyo wakati Bunge la kumi lilopita,ambapo kwa sasa alijiapiza kurudi tena kwenye nafasi hiyo nyeti ndani bunge ambapo inaonekana ni kama ndoto yake imeota mbawa.
    Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya Ofisi za Bunge ambazo mtandao huu umezipata zinasema Spika  Job Ndugai ameshamaliza kupanga safu  kwenye kamati mbali mbali, kabla haja wasilisha majina hayo,kwenye kamati  itakayokutana kesho  ijumaa ya tarehe 15  kwenye kikao cha kamati itakachofanikia ofisi ndogo za Bunge zilizopo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupitisha majina hayo ya viongozi wa kamati mbali mbali za Bunge na wajumbe wake,
Ambapo inatakatiwa wajumbe wa kamati na wenyekiti wake kumalizika  na uteuzi wake kabla ya kikao cha Bunge akijaanza tarahe 26 ya mwezi huu.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu huyo ameuambia mtandao huu jina la zitto Kabwe limeenguliwa kwenye kamati ya (PAC) kwa kile kinachoitwa ni kutokana na tuhuma mbali mbali alizotumiwa wakati akiwa mwenyekiti wa (PAC).
“Spika Ndugai alishakamilisha safu yake siku nyingi sana,katika safu za kamati ndani ya Bunge,kuhusu PAC jina la zitto alipo lilishaondolewa kabisa,nakuapia kabisa ndugu huyu Ziito ategemee Mungu tu kurudi kwenye Kamati ya PAC”Kimesema Chanzo chetu hicho.
        Inadaiwa Zitto anatarajiwa kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati moja wapo tofauti na PAC ambapo mtoa taarifa wetu aligoma kutaja kwa kusema ni bado mapema huku akimtaka mwandishi wa mtandao kuwa na subira.
      Sababu inayotajwa na vyanzo mbali mbali kutoka ndani ya Bunge ni kuwa Spika Ndugai amefikia uamuzi huo wa kumwondoa Zitto Kabwe kwenye PAC  inatokana na wabunge wenzake haswa wa Upinzani kujiandaa kumgomea zitto kurudi nafasi hiyo baada ya kutuotuhuma mbali mbali anazotuhimiwa wakati akiwa kiongozi wa kamati hiyo,
    Tuhumu hizo ni ile ya kuilinda serikali wakati Kamati yake ilipokuwa inachambua  ripoti ya uchunguzi iliyofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wakati ilipokuwa inachunguza sakata la uchotwaji wa mabilioni ya escrow iliyokuwa ndani ya Benki kuu B.OT,
Ambapo Zitto Kabwe anatuhumiwa kwake kwa kushindwa kutaja majina ya Vigogo waliopewa mgao  wa fedha na anayejiita na Kuitwa  mmiliki wa kampuni ya Pan Africa Power Solutions Tanzania Limited (PAP) bwana Seith kwenye Benki ya stanbink ambao inadaiwavigogo wakubwa wa serikali pamoja na watendaji wa kipindi kile wa Ikulu walinufaika na mgao huo
,Huku Zitto akaishia kuwataja wahusika walipewa mgao na mmiliki wa  kampuni ya Engineering and Marketing Limited (VIP) James Rugemalira kupitia Benki ya Mkombozi.
   “Zitto huyu mwenyewe amejiaharibia wakati akiwa mwenyekiti wa PAC alikubali kuwatoa kafara wakina Tibaijuka watu ambao hata hawaijuia Escrow yenyewe,akawafumbia macho vigogo wa Stanbick huku ndiko hadi watu wa ikulu walikula, ambapo kamati yake PAC ilikuwa na Nguvu ya kuitaka TAKUKURU kuwapa majina ili wajulikane wakina nani lakini yeye hakufanya hivyo sasa leo ndio anavuna alichopanda kabisa na Spika kaangalia huyu mtu aaminiki”
Alipotafutwa Zitto Kabwe ili ajibu hatua hii ya Spika kuliondoa jina lake,simu yake Haikuweza kupatikana.


Akizungumzia hatua ya Spika Ndugai kuliindoa jina lake,Mchambuzi wa masuala ya kisiasa kutoa chuo kikuu cha Dodoma William Alocye amesema hatua hiyo itakuwa pigo kubwa kwa Zitto Kabwe.
“Yaani hapo naiona dalili ya zitto kabwe kupotea umaarufu wake,maana kamati hiyo imempa umaarufu sana na pia sio hivyo tu hata kipesa amenufaika maana hapo kuna mengi sana yamefichika ndugu huyo anakagua mashirika ya umma unategemea nini kwa mashirika ya umma yanavyonuka ufisadi hivyo yeye unategemea naye asinufaike”amesema Alocye.





Hakuna maoni