Zinazobamba

ZITTO KABWE AIAMSHA IKULU YA MAGUFULI,SASA BENK YA STANBINK YAINGIA MATATANI TENA,SOMA HAPO KUJUA

OM1
Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue akiongea na Waandishi wa Habari leo 01 Disemba, 2015 katika Ofisi ya Mawasiliano Ikulu kuhusu Tanzania kurejeshewa dola za Marekani milioni 7 katika kesi iliyofunguliwa katika Mahakama Jijini Uingereza dhidi ya Benki ya Stanbink Tanzania.

NA KAROLI VINSENT
BENKI ya Stanbink iliyokuwa inatumika kuchota pesa na  watuhumiwa wa Ufisadi kwenye sakata la  Akaunt ya Tegeta Escrow  iliyokuwa ndani ya Benki kuu ya Tanzania,B.OT,sasa Benki hiyo imeingia matatani tena baada ya Ikulu kuibuka na kuitaka kuilipa serikali ya Tanzania fidia,
 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam leo kuhusiana na tuhuma zilizoelekezwa benki ya Stanbic Tanzania kuwa imetumika katika kufanya udanganyifu wa riba ya mkopo dola Milioni 600 iliyopewa serikali ya Tanzania na Uingereza kupitia Kampuni ya Egma ya Tanzania.

Kashfa hiyo ambayo iliibuliwa na Mbunge wa Kigoma Mijini kupitia Chama cha ACT-Wazalendo,Zitto Kabwe jana kupitia kwenye Vyombo vya Habari ambapo aliitaka serikali kuingilia kati,
       Ambapo Sefue  amesema kuwa Benki kuu ilifanya ukaguzi wa benki hiyo na mambo mengine walibaini malipo yasiyokuwa ya kawaida kuhusiana na kampuni ya kitanzania inayoitwa Egma,malipo hayo yalikuwa kinyume na taratibu za kibenki na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo walishindwa kuvumilia kwa hiyo tetesi tukazipata, wakaguzi wa benki kuu walifuatilia,

 malalamiko hayo na kujiridhisha kuwa uongozi wa benki ya Stanbic Tanzania ulifanya mambo ambayo ni kinyume na taratibu zinazokubalika kibenki, ambapo fedha kiasi cha dola milioni 6 ziliingizwa kwenye kampuni ya Kampuni ya Egmwa na siku chache zilitolewa zote kwa fedha taslimu wala benki haikukusanya kodi ya zuio ambayo kwa mujibu wa sheria ya kodi ilipaswa kutozwa.

Hakuna maoni