YANGA YAANZA KUSHIKANA UCHAWI NA WACHEZAJI,YAMTIMUA HARUNA NIYONZIMA,SOMA HAPO KUJUA
Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima (kulia) akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Abdallah Bin Kleb |
YANGA SC imevunja
Mkataba na kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima kutokana na mchezaji
huyo wa Amavubi kukiuka vipengele vya mkataba wake na klabu hiyo. Anaandika
Erasto Masalu … (endelea).
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha
amewaambia Waandishi wa Habari katika Mkutano uliofanyika makao makuu ya klabu,
Jangwani, Dar es Salaam kwamba Niyonzima pia atatakiwa kuilipa
klabu.
Niyonzima amekuwa
katika mgogoro na klabu ya Yanga kwa muda mrefu toka alipochelewa kujiunga na
klabu yake, akitokea kwao kuitumikia timu ta Taifa ya Rwanda katika michuano ya
kimataifa mapema mwezi huu.
Yanga imefikia uamuzi
huyo baada ya kumsimamisha nyota huyo kipenzi cha Wanajangwani, lakini pia
ilimhoji kupitia Kamati yake ya Nidhamu na kumpa nafasi kiungo huyo kujieleza.
Maoni 1
Tafadhalini Simba msimwache mchezaji huyo almasi
Chapisha Maoni