Zinazobamba

WAZIRI WA MAGUFULI AMUUMBUA KIKWETE,NI KUHUSU MAJINA YA VIGOGO WAUZA MADAWA YA KULEVYA NCHINI,SOMA HAPO KUJUA


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini.

NA KAROLI VINSENT
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya nchi, Charles Kitwanga ni kama amemruka Rais mstaafu Jakaya Kikwete kuhusu uwepo wa orodha ya majina ya vigogo wanaouza madawa ya kulevya nchini, baada ya kusema hakuna orodha ya majina hayo,

Hata hivyo pia Waziri Kitwanga amewatangazia kihama,  watu wote wanajihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya nchini kwa kusema hata muogopa mtu yeyote na iwe mkubwa wala mdogo wote atawachukulia hatua.

     Akizungumza na waaandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumalizika  mazungumzo  na viongozi  wakuu wa jeshi la polisi nchini,ambapo Waziri Kitwanga amesema kwa sasa hakuna orodha yeyote ya majina ya vigogo wanaojihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya, kwa kudai kuwa kama orodha hiyo ingekuwepo basi angeshawachukulia hatua za kisheria.

      “Hakuna orodha ya wauza madawa ya kulevya hapa au hao wanaoitwa vigogo,maana kama wangekuwepo ningewachukulia hatua, maana simwogopi mtu kabisa awe mkubwa au mdogo kama unajihusisha na biashara hii lazima tukuchukulia hatua”amesema Waziri Kitwanga.
      Waziri Kitwanga ameongeza  kuwa kwa sasa wizara yake pamoja na kushirikiana na kitengo cha kupambana na biashara ya madawa ya kulevya nchini wametaka watu wote wanaofanya biashara hizo kuachana mara moja.
      “Nawataka kabisa  watu wote wanaojihusisha na biashara ya kuuza madawa ya kulevya waache kabisa na wafanya kazi nyengine maana tumejipanga kupambana nao kufa na kupona na kuhakikisha tunamaliza kabisa mtandao wote nchini”ameongeza kusema.
   Kuibuka huku kwa Waziri Kitwanga kunakuja ikiwa na miaka minane kupita wakati wa kipindi cha utawala wa awamu ya nne ambapo Rais Kikwete aliliambia taifa kuwa anamajina ya vigogo ya wauza madawa ya kulevya nchini na kujiipiza kuwa atawachulia hatua kali za kisheria.

       Jambo ambalo mpaka Kikwete anaondoka madarakani hakuna hata kigogo mmoja aliyemchukulia hatua au kumfikisha mahakamani zaidi tu ya wauzaji wadogowadogo maarufu kama  vidagaa tu ndio wakifikishwa mahakamani huku vigogo wakitesa,

     Kauli ya waziri Kitwanga inatafsiriwa na wachambuzi wa mambo ni kama inamuumbua Rais mstaafu Kikwete kwa kuonesha alikuwa hana majina hayo sana sana alikuwa anataka sifa au huruma kwa wananchi.

  IGP MANGU ANENA.
Katika hatua nyengine Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,Ernest Mangu ametangaza kumsaka mtu aliyesambaza ujumbe kwenye mitandao ya kijamii akisema jeshi la polisi limewasimamisha wafanyakazi wake 300 kwa madai ya kugushi vyeti.

“Taarifa ambazo hizo ni za uongo,na kwa sahivi tunamtafuta mtu alisambaza ujumbe huo ili tumchukulie hatua za kisheria”amesema IGP,Mangu.

Hakuna maoni