Zinazobamba

WAZIRI KITWANGA AWASHUKIA WATENDAJI WA UHAMIAJI NCHINI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi,Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa Habari hawapo pichani leo mara baada ya kumaliza kikao na watendaji wa Idara ya Uhamiaji nchini
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi,Charlse Kitwanga ameitaka Idara ya Uhamiaji kutompa mgeni yeyote kibali cha kuishi nchini bila mgeni huyo kutokuwa na kibali cha kufanya kazi  nchini.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
    Akizungumza na waaandishi leo Jijini Dar es Salaam, mara baada ya kumalizika kikao na makamishna watendaji wa Idara ya Uhamiaji nchini,Waziri Kitwanga amesema kwa sasa kumekuwa na msuguano kati ya Idaya ya uhamiaji ambao ndio wanatoa kibali cha kuishi nchini na wizara ya Kazi ambao wanatao kibali cha kufanya kazi kwa wageni nchini.
“Nimewataka idara ya uhamiaji nchini kutompa mgeni yeyote kibali cha kuishi nchini,mpaka wizara ya kazi watakapompa kibali cha kufanya kazi nchini mgeni ,kwasababu kumekuwa na wageni ambao wamejaa nchini ambao hawana shughuli za kufanya jambo linaloweza kuleta uharifu”Amesema Waziri Kitwanga.
     Waziri Kitwanga ameongeza kuwa katika kukabiliana na tatizo la rushwa kwa watendaji wa uhamiaji amesema kwa sasa wizara yake pamoja na idara hiyo wako mbioni kuanzisha mfumo mpya wa utoaji pasi za kuishi, bila ya mwananchi kutoonana na mtumishi wa uhamiaji,
     Ameeleza kuwa mfumo huo ambao utamfanya mwananchi kujiorodhesha na kufuata hatua zote ikiwemo kwenda kulipa benki kwa kutumia kupyuta jambo analodai litachangia kuaondoa Rushwa kabisa,

     Aidha,Waziri Kitwanga ameunda timu ya watu wa uhasibu kutoka wizarani kwake kwenda kufanya uchunguzi wa matumizi ya fedha katika idaya ya uhamiaji lengo ni likiwa kuzima mianya ya pesa inayopetea katika idara hiyo.

Hakuna maoni