Zinazobamba

VYUO VIKUU NCHINI HATARINI KUFUNGWA,PROFESA MKUMBO AMUANGUKIA MAGUFULI,SOMA HAPO KUJUA


Pichani ni Prifesa Kitila Mkumbo
VYUO vikuu nchini vimetajwa kuwa  viko hatarini kufungwa kutokana na  kukosa Wanafunzi.Anaadika KAROLI VINSENT endelea nayo.
     Tahadhari hiyo imetolewa na Mhadhili kutoka chuo kikuu cha Mlimani,Profesa Kitila Mkumbo wakati wa kuwasilisha mada kwenye uzinduzi ya ripoti iliandaliwa na Taasisi ya Haki ya Elimu kuhusu maendeleo ya elimu yalitokelezwa na  awamu iliyomalizika ua Rais Jakaya Kikwete ndani ya miaka kumi,
        Profesa Mkumbo amesema kutoka na idadi ndogo ya wanafunzi wanaomaliza kidato cha sita  huku vyuo vikuu kuwa vingi basi kutaleta hatari kubwa ya vyuo  vikuu kufungwa,
       Amebainisha  kuwa asilimia 25 tu ya wanafunzi ndio wanakwenda kwenye vyuo vikuu huku idadi kwenda chuo kikuu,huku wengine wakikosa sifa ya kuchaguliwa kwenda kwenye vyuo hivyo,pamoja na Ada za masomo jambo analodai kuwa limechangia vyuo vingi vikuu kukosa wanafunzi.
      Hata hivyo,Profesa Mkumbo ameishauri Serikali ya awamu ya Tano chini ya  Rais John Magufuli kuliangalia suala hilo kwa umakini ili kuweza kuliokoa Taifa kwenye sekta ya elimu hususani suala la Udahili wa wanafunzi.
     Naye Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema ambaye alikuwa Waziri kivuli wa Wizara ya Elimu kwenye utawala wa awamu ya nne,Suzan Lyimo amsema hali  ya elimu kwa sasa nchini ipo katika hali mbaya baada ya serikali kushindwa kusimamia elimu kwa dhati,
    Amesongeza kusema kuwa kutokuwa na vyuo bora vya ufundi nchini ni tatizo,huku akimtupia lawama Rais mstaafu Jakaya Kikwete kushindwa kutekeleza ahadi yake ya kujenga vyuo vya ufundi kila kata.
    Kwa upande wake Mkurugenzi wa Haki Elimu John  Kalage amesema ili elimu iokolewe hapa ilipo ni kwa serikali kuangalia kwa umakini Bajeti ya Elimu nchini kwa kuondoa matumizi makubwa yasiyo na lazima badala yake pesa hizo zielekezwe kwenye masuala ya maendeleo ya elimu.




Maoni 1

Abdallah the Write alisema ...

Dahh hivi ni lazima kila mtu awe anaandika mbona kilichoandikwa hakieleweki?