Zinazobamba

POLISI WAUANA WENYEWE KWA WENYEWE KISA MAPENZI,SOMA HAPO KUJUA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha
Polisi Mwanza amuua mwenzake na kujiua
         
HALI isiyokuwa ya kawaida, askari Polisi wawili wamefariki dunia katika Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, baada ya mmoja wapo kumpiga risasi mwenzake kisha na yeye kujipiga risasi. Anaandika Moses Mseti, Mwanza … (endelea).
Tukio hilo limetokea leo saa 8:30 mchana katika eneo la benki ya Posta iliyopo barabara ya Nyeyere, baada ya askari polisi aliyekuwa amevalia kiraia kufika kwenye benki hiyo kupata huduma ambapo ndipo tukio hilo likatokea.
Pia inadaiwa kuwa polisi hao walifikia hatua hiyo baada ya kudaiwa kuwepo kwa ugomvi wa muda mrefu ambao unadaiwa unatokana na wivu wa kimapenzi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa marehemu aliyejiuwa hakuwa na tatizo lolote la kiafya na wala wakati wote hakuonekana kuwa na msongo wa mawazo.
Kamugisha alimtaja askari aliyempiga risasi mwenzie kisha na yeye kujiua kuwa ni namba H. 852 PC Masunga Elisha, ambaye alikuwa na mwenzake namba H. 4291 PC Remigius Alphostin kwenye lindo la benki ya Posta jijini Mwanza.
Pia Kamugisha alimtaja marehemu aliyepigwa risasi kuwa ni namba H. 5950 PC Petro Matiko, ambaye alifika katika eneo hilo la benki kupata huduma ambapo ndipo tukio hilo la kusikutisha kutokea.
“PC Matiko (marehemu Petro Matiko) alifika katika eneo la benki kupata huduma za kibenki lakini baada ya kutoka ndani alisalimiana na wenzake na kuwaeleza kwamba mtandao unasumbua, huku akimuuliza kwanini unaikoki silaha unafahamu kama ni hatari lakini PC Masunga alimwambia aachane nae ndipo akampiga risasi,” amesema Kamugisha.
Hata hivyo baada ya PC Masunga kutekeleza tukio hilo pia na yeye alijipiga risasi katika eneo la kidevu karibu na mdomoni na kupoteza maisha papo hapo.
Kamanda Kamugisha amesema kuwa mpaka sasa chanzo cha tukio la askari hao kufanya tukio hilo hakijafahamika na kwamba wanaendelea na uchanguzi wa tuki hilo.
Mashuhuda.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo, Marwa Ezekiel na Neema Daud, wamesema kuwa baada ya kusikia mlio wa risasi baadhi ya wateja waliokuwa katika benki hiyo walianza kufunga mlango wa kuingia benki.
Pia wamesema kuwa baada ya dakika tano kupita walisikia mlio mwingine wa risasi wakati walipotoka nje walimuona askari aliyejiua akiwa amelala karibu na mlango huo wa kuingia katika benki hiyo.

“Sisi tulikuwa ndani ya benki lakini wakati tukiendelea na huduma ghafla tulisikia mlio lakini baada ya dakika tano tukasikia mlio mwingine ndipo watu wakaingia ndani,” amesema Neema Daud.
Hata hivyo amesema kuwa wakati mlio wa risasi ya kwanza unasikika walizani ni mlio wa pikipiki lakini baada ya kusikia mlio wa pili ndipo wakatoa nje na kuona marehemu hao wakiwa wamelala chini.

Watu wa karibu na marehemu
Hata hivyo baadhi ya watu wa karibu na marehemu hao, ambao hawakutaka majina yao kuandikwa kwenye gazeti walisema kuwa marehemu hao walikuwa na ugomvi wa muda mrefu huku wengine wakilihusisha tukio hilo na masuala ya kuzulumiana fedha.
“Hawa jamaa (marehemu wawili) hawawezi kufanyiana tukio la namna hii, ukiangalia kwanza yule aliyepigwa risasi (Petro Matiko) wakati alipoingia ndani hakuwaongelesha lakini alipotoka ndipo akawaeleza mtandao unasumbua hapo lazima kuna kitu,” amesema mtu ambaye hakutaka kutajwa kuandikwa jina lake.
Hata hivyo alidai kwamba awali walikuwa wakisikia kwamba marehemu hao wanadaiana fedha hivyo hawakufahamu ni kiasi gani na walikopeshana namna gani.
Tukio hilo la Polisi kuua mwenzake na kisha yeye kujiua limegusa hisia tofauti kwa wakazi wa Jiji la Mwanza, ambapo watu waliozungumza na gazeti hili wasema kuwa tukio hilo ni la mara ya kwanza kutokea katika mkoa huo.
Abdalah Hussein na Elisha Hezron ni wakazi wa jijini hapa wamesema kuwa tukio lazima jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kwani askari aliyepitia mafunzo hawezi kufanya tukio la namna hiyo.
“Kwanza ni kitu ambacho hakiingii kichwani kwangu na hata kwa watu wengine hivi askari aliyepitia mafunzo kupiga risasi mbele ya watu tena benki, uchunguzi unapaswa kufanyika wa kina,” amesema Hussein.



Hakuna maoni