Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-MAKONTENA 11,884 NA MAGARI 2,019 VYAPOTEA BANDARINI TENA,KAMPUNI YA AZAM NA WENZAKE WAZIDI ITAFUNA NCHI,WAZIRI MBARAWA AISHIWA PUMZI,SOMA HAPO KUJUA

WAZIRI wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame mbarawa ameibua ufisadi wa kutisha ndani ya Mamlaka ya Bandari nchini TPA,baada ya kubaini  upotevu wa makotena 11,884 pamoja na magari 2,019 kwenye Bandari kavu 7.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
    Waziri Mbarawa ameyaibua hayo leo alipofanya ziara ya kushtukiza ndani ya (TPA) ambapo  amesema mara baada ya Waziri mkuu,Kassim Majaliwa kufanya ziara Bandarini hapo mwezi mmoja uliopita alibaini upotevu wa Makotena 2431yalikuwa kwenye Bandari kavu,
      Amedai kuwa Baada ya Majaliwa kubaini upotevu akaiamulu TPA kufanya ukaguzi wa kina,ambapo  leo uchunguzi huo umebaini kuna upotevu  wa Makontena mengine  11,884 yenye thamani  ya bilioni 48  na magari 2019 yenye thamani ya bilioni 1 yakiwa yamepita bila  kulipwa tozo (wharfage).
         Waziri Mbarawa amezitaja Bandari kavu hizo zilizohusika na Kashfa hiyo  ni ya  Azam yamepotea 295 , PMM makontena 779,Kampuni ya JEFAG makontena 1450,TRH makontena 4,424,AMI makontena 4,384,
Makampuni  mengine ni MOFED makontena 61 pamoja na Kampuni ya DICD 491,
    Sanjari na Upotevu huo wa Makontena pia Waziri Mbarawa ameyataja makampuni mengine yalihohusika na upotevu wa Magari 2,019  ni TALL 309,CHICAS magari 65,HESU 1,359,SILVER magari 97.

  HATUA ZILIZOCHUKULIWA.
     Waziri Mbarawa amesema baada ya kubaini upotevu hadi kufikia leo  Desemba 29 mwaka huu watumishi 7 kati ya 15 waliokuwa wamehusika na ukusanyaji wa mapato ya Wharfage katika ICD na CFS wamekamatwa na kufikishwa polisi ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria huku wengine nane wakitafutwa.
 Sanajari na hatua kwa watumishi hao pia,Waziri Mbarawa amewapa siku 7 makapuni ya uwakala 243 yaliohusika na upotevu huo wawe wamelipa kodi hizo,
Vilevile Waziri Mbarawa amesema Serikali ya awamu ya tano haita mvumilia mfanyakazi yeyote wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania awe mkebwa au mdogo ambaye ataendelea kujihusisha na upotevu wa mapato basi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Hakuna maoni