Zinazobamba

WIZARA YA NISHART YAISHUKIA TANESCO KWA WATEJA WANAOIBA UMEME,SOMA HAPO KUJUA

pichani ni Afisa habari kutoa Wizara ya Nishart na Madini,Badra Masoud katika ukumbi wa habari maelezo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa taarifa yake kuhusu wizi wa Umeme


IKIWA ni dalili za Serikali ya Rais Joh Magufuli kuanza kukusanya kodi kwa kubana mashitika ya umma ni kama imeanza baada ya SERIKALI kuliagiza shirika la TANESCO kuimarisha kikosi chake cha ukaguzi wa watumiaji wa umeme ili kubaini wateja wasio waaminifu wanaoiba umeme pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria. Anaandika KAROLI VINSENT ... (endelea).
Hayo yamesemwa leo na msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud katika ukumbi wa habari maelezo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa taarifa yake kuhusu wizi wa Umeme.
Masoud amesema wizara yake inatarajia kuunda kikosi maalum kitakachojumuisha wataalam kutoka TANESCO na vyombo vya usalama kwa lengo la kukabiliana na tatizo hilo linalokosesha mapato shirika la TANESCO.
Amesema kuwa sambamba na kulitaka shirika hilo kukabiliana na wizi wa umeme, amezitaka pia taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali kuzingatia matumizi bora ya Umeme ili kudhibiti upotevu wa nishati hiyo muhimu. Utaratibu huo pia hufanywa na nchi nyingi Duniani kwa lengo la kukabiliana na upotevu wa umeme.
Masoud ameeleza kuwa hatua hiyo imekuja baada ya taasisi kuona kwamba taasisi mbalimbali huwa zinaacha umeme ukiendelea kupotea baada ya muda wa kazi.
Ameya horodhesha baadhi ya matumizi hayo ya vifaa ambavyo huviacha vikiendelea kufanya kazi hata kwa muda ambao sio wa kazi, kama vile AC, taa, kompyuta na baadhi ya vifaa vingine vinavyotumia umeme.
Akizungumzia hali ya umeme hapa nchini, Masoud amesema hakuna mgawo wowote unaoendelea hivi sasa kwani hali ya uzalishaji ni nzuri pamoja na mabwawa ya maji ambayo hutumika kuzalisha umeme kukauka lakini kiasi kikubwa cha umeme kinachozalishwa kwa sasa kinatokana na Gesi asilia ambapo kiasi kidogo kinazalishwa kwa kutumia mabwawa ya maji.
kiasi cha umeme kinachopatikana kwasasa ni megawati 1500 huku matumizi ikiwa ni kati ya megawati 800 na 900 kwa siku.” Amesema Masoud.



No comments