WAANGALIZI WA TACCEO WAZIDI TESEKA POLISI NI WALE WALIOVAMIWA NA POLISI NA KUPORWA VITU VYAO,SOMA HAPO KUJUA
Wafanyakazi wa kituo cha sheria na haki za
binadamu nchini Tanzania LHRC ambao walikuwa wanafanya uangalizi wa uchaguzi
kupitia mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini TACCEO
wameendelea kusota polisi baada ya leo kufanyiwa mahojiano ya awamu ya pili
kuhusu tuhuma mbalimbali zinazowakabili.
Wafayakazi hao wapatao 38 walikamatwa na jeshi la
polisi wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu nchini huku vifaa vyao pia
vikikamatwa kwa tuhuma za kusambaza habari za uchaguzi mkuu kinyume na sheria
za uchaguzi na katiba ya Tanzania.
Akizungumza na wanahabar ndani ya makao makuu ya
polisi nchini Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam SULEMAN KOVA
amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea kuwahoji wafanyakazi hao 38 wa kituo
cha sheria na haki za binadamu kwa tuhuma za kukusanya na kusambaza taarifa
zisizo sahihi kwenye mitandao ya kijamii kinyume na kifungu namba 16 cha sheria
inayodhibiti makosa ya kimtandao.
Kamishna KOVA amesema kuwa wakati wa harakati za
kusubiri matokeo ya uchaguzi mkuu uliomalizika hivi karibuni zilipatikana taarifa
za kuaminika kuwa kituo hicho kilikuwa kinajihusisha na upokeaji wa matokeo
kutoka vituo mbalimbali vya kupigia kura kutoka kwa mawakala wao waliowaweka
nchi nzima na hatimaye kusambaza taarifa hizo kwa watu wasiohusika ikiwemo
mitandao ya kijamii ambapo amesema kuwa kisheria kazi ya kupokea na kusambaza
matokeo ni ya tume ya taifa ya uchaguzi pekee.
Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam SULEMAN KOVA akizungumza na wanahabari nkuhusu sakata hilo |
Amesema katika mahojiano ya awali polisi waligundua
kuwa kituo hicho kilipewa kibali na tume ya taifa ya uchaguzi kuwa waangalizi
wa ndani wa uchaguzi ambapo walipewa masharti ya namna ya kuendesha kazi zao
ikiwa ni pamoja na kutotoa maoni na taarifa yoyote kwa vyombo vya habari au
umma juu ya mchakato wa uchaguzi wakati wa zoezi la kupiga kura likiendelea au
kutofanya majukumu ya kiutendaji ya tume ya taifa ya uchaguzi chini ya kifungu
namba 12 cha maelekezo kwa waangalizi wa ndani na wanje wa uchaguzi 2015.
Amesema kuwa polisi wamegundua kuwa wamekuwa
wakikiuka masharti na sheria hizo hivyo wamewaita ili kuweza kuwafanyia
mahojiano zaidi ili wakipatikana na hatia sheria iweze kuchukua mkondo wake
ikiwa ni pamoja na kupeleka jalada hilo kwa mwanasheria mkuu wa serikali
na kama kuna wengiune watakutwa hawana hatia wataachiwa huru wao pamoja na
vifaa vyao
LHRC WAZUNGUMZA.
Akizungumza na wanahabari nje ya makao makuu ya
polisi mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu HELLEN KIJO
BISIMBA amesema kuwa baada ya wafanyakazi wao kufanyiwa mahijiano ya mara ya
kwanza leo wameitwa tena kwa ajili mahojiano ya nyongeza juu ya sakata hilo
hivyo vijana wake wameitika wito huo.
Amesema kuwa kituo chake kimeathirika sana na tukio
hilo kwani limefanya kazi za wanaharakati hao zimesimama kwa muda usiojulikana
huku vifaa na vitendea kazi vyao vikiwa vimeshikiliwa na jeshi la polisi huku
wakiwa hawajui hatma ya sakata hilo kwa ujumla.
Tukio la kukamatwa kwa wafanyakazi wa kituo hicho ni
tukio la pili baada ya tukio la kwanza lililotokea huko njombe kipindi cha
uandikishwaji wa BVR ambapo Bi HELLEN KIJO BISIMBA amesema haelewi ni tatizo
gani linawakumba kwani wanafanya kazi kwa mujibu wa shetia na wakiwa na vibali
vyote vya kufanya kazi za uangalizi.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni