Zinazobamba

WAANGALIZI WA TACCEO WAZIDI TESEKA POLISI NI WALE WALIOVAMIWA NA POLISI NA KUPORWA VITU VYAO,SOMA HAPO KUJUA



Mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za Binadamu nchini LHRC Bi HELEN KIJO BISIMBA akiongoza wafnayakazi wa kituo hicho Wakitoka makao makuu ya jesho la polisi mchana wa leo wakati mahojiano ya vijana wao 38 waliokamatwa yakiendelea
Wafanyakazi wa kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC ambao walikuwa wanafanya uangalizi wa uchaguzi kupitia mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini TACCEO wameendelea kusota polisi baada ya leo kufanyiwa mahojiano ya awamu ya pili kuhusu tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

Wafayakazi hao wapatao 38 walikamatwa na jeshi la polisi wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu nchini huku vifaa vyao pia vikikamatwa kwa tuhuma za kusambaza habari za uchaguzi mkuu kinyume na sheria za uchaguzi na katiba ya Tanzania.

Akizungumza na wanahabar ndani ya makao makuu ya polisi nchini Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam SULEMAN KOVA amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea kuwahoji wafanyakazi hao 38 wa kituo cha sheria na haki za binadamu kwa tuhuma za kukusanya na kusambaza taarifa zisizo sahihi kwenye mitandao ya kijamii kinyume na kifungu namba 16 cha sheria inayodhibiti makosa ya kimtandao.

 
Kamishna KOVA amesema kuwa wakati wa harakati za kusubiri matokeo ya uchaguzi mkuu uliomalizika hivi karibuni zilipatikana taarifa za kuaminika kuwa kituo hicho kilikuwa kinajihusisha na upokeaji wa matokeo kutoka vituo mbalimbali vya kupigia kura kutoka kwa mawakala wao waliowaweka nchi nzima na hatimaye kusambaza taarifa hizo kwa watu wasiohusika ikiwemo mitandao ya kijamii ambapo amesema kuwa kisheria kazi ya kupokea na kusambaza matokeo ni ya tume ya taifa ya uchaguzi pekee.

Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam SULEMAN KOVA akizungumza na wanahabari nkuhusu sakata hilo

Amesema katika mahojiano ya awali polisi waligundua kuwa kituo hicho kilipewa kibali na tume ya taifa ya uchaguzi kuwa waangalizi wa ndani wa uchaguzi ambapo walipewa masharti ya namna ya kuendesha kazi zao ikiwa ni pamoja na kutotoa maoni na taarifa yoyote kwa vyombo vya habari au umma juu ya mchakato wa uchaguzi wakati wa zoezi la kupiga kura likiendelea au kutofanya majukumu ya kiutendaji ya tume ya taifa ya uchaguzi chini ya kifungu namba 12 cha maelekezo kwa waangalizi wa ndani na wanje wa uchaguzi 2015.

Amesema kuwa polisi wamegundua kuwa wamekuwa wakikiuka masharti na sheria hizo hivyo wamewaita ili kuweza kuwafanyia mahojiano zaidi ili wakipatikana na hatia sheria iweze kuchukua mkondo wake ikiwa ni pamoja na kupeleka jalada  hilo kwa mwanasheria mkuu wa serikali na kama kuna wengiune watakutwa hawana hatia wataachiwa huru wao pamoja na vifaa vyao

LHRC WAZUNGUMZA.

Akizungumza na wanahabari nje ya makao makuu ya polisi mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu HELLEN KIJO BISIMBA amesema kuwa baada ya wafanyakazi wao kufanyiwa mahijiano ya mara ya kwanza leo wameitwa tena kwa ajili mahojiano ya nyongeza juu ya sakata hilo hivyo vijana wake wameitika wito huo.

Amesema kuwa kituo chake kimeathirika sana na tukio hilo kwani limefanya kazi za wanaharakati hao zimesimama kwa muda usiojulikana huku vifaa na vitendea kazi vyao vikiwa vimeshikiliwa na jeshi la polisi huku wakiwa hawajui hatma ya sakata hilo kwa ujumla.

Tukio la kukamatwa kwa wafanyakazi wa kituo hicho ni tukio la pili baada ya tukio la kwanza lililotokea huko njombe kipindi cha uandikishwaji wa BVR ambapo Bi HELLEN KIJO BISIMBA amesema haelewi ni tatizo gani linawakumba kwani wanafanya kazi kwa mujibu wa shetia na wakiwa na vibali vyote vya kufanya kazi za uangalizi.


Hakuna maoni