Zinazobamba

UCHAGUZI WA KATA YA SARANGA MANISPAA YA KINONDONI RASMI JUMAPILI,SOMA HAPO KUJUA


MANISPAA ya Kinondoni imewataka wakazi wa kata  saranga ambayo haikufanya uchaguzi kwa ngazi ya Diwani kujitokeza siku ya jumapili ya tarehe 15 mwezi huu kwa ajili ya kupiga kura ili kumchagua diwani wanaomtaka.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
        Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Eng. Mussa Natty amesema taratibu za maandalizi ili kulekea siku ya uchaguzi umekamilika kwa kuandaa vifaa vyote vya uchaguzi wa ngazi ya Udiwani,
      Amesema Uchaguzi huo ambaoulitarajiwa kufanyika Octoba 25 mwaka huu ulihairishwa kutokana na kuwepo dosari kadhaa.
        Amezitaja Dosari hizo zilizopelekea uchaguzi kuhairishwa ni kutokea kwa vurugu kubwa siku  ya kupiga kura
“Mnamo saa 11 asubuhi siku hiyo ya tarehe 25 Octoba ambayo ilikuwa ni siku ya kupiga kura baadhi ya wasimamizi na watu wasiojulikana  kufika katika eneo la ugawajwi wa vifaa vya uchaguzi iliopo eneo la TANROAD Temboni”
Amesema baada hali hiyo kutokea ndipo baadhi ya vifaaa vilipotea kutokana na vurugu hizo,
Sanjari na vurugu hizo Eng Natty ametaja kasoro zengine ni kuwepo na upungufu wa karatasi  za kupigia kura jambo lilowafanya kuhailisha uchaguzi huo.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo,amewataka wakazi ya kata Saranga kujitokeza kwa wingi siku ya Jumapili ili waweze kumchagua Kiongozi wa ngazi ya Diwani.

Ambapo amesema Manispaa yake imeafanya juhudi kubwa ya kuwataharifu wakazi wa kata ya saranga kwa kutumia magari kutoa taarifa.

No comments