Zinazobamba

SHEIKH PONDA AKWAMA TENA,AZIDI SOTEA KESI YAKE,SOMA HAPO KUJUA

ponda

MAHAKAMA ya hakimu mkazi Morogoro,kwa mara nyengine tena imehairisha hukumu ya kesi Jinai inayomkabili kiongozi wa Taasisi ya Dini ya Kiislam nchini ,Sheikh Ponda Issah Ponda.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo,
Kesi hiyo ilitarajiwa kutolewa hukumu leo  Jumatano na Hakimu Makazi wa Mahakama hiyo,Mery Moyo,imehairishwa na Mtuhumiwa amerejeshwa Rumande baada ya kuelezwa hakimu kutokewepo Mahakamani kutokana na  kwenda kwenye kozi fupi ya kusimamia kesi za uchaguzi Mjini Dodoma.
Ambapo shauri hili limehairishwa hadi tarehe 30 ya mwezi huu Novemba na Hamimu Mkazi ,Erick Rwechumbiza ambapo siku hiyo mtuhumiwa atafikishwa mahakamani hapo.
Mshtakiwa huyo anakabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo kushawishi wa imani wa dini ya Kiislam nchini kutenda makosa,ambayo anadaiwa kutenda kosa Ogost 2013,
Upande wa mashtaka uliwakilishwa na wakili wandamizi wa Serikali Berdard Kongola,Sunday Hrela na George Mbalasa wakati wa upande wa Mshtakiwa unawakilishwa Wakili Juma Nasoro ,Abubakal Salim na Bartholomeo Tarimo.

Awali kesi hiyo ilipangwa kutolewa hukumu 19 ya mwezi wa kumi ambapo shauri hilo lilihairishwa hadi Novemba 18 , ya leo,ambapo tena limepigwa kalenda haki Novemba 30 ya mwezi huu,

No comments