Zinazobamba

MAGUFULI KUKIONA SASA,UKAWA WAAPA KUFIA BUNGENI IJUMAA HII,TUNDU LISSU ASEMA PATACHIMBIKA MPAKA ZANZIBAR KIELEWEKE,SOMA HAPO KUJUA




Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umesema utakuja na stahili mpya wakati  Rais Dk. John Magufuli, atakapokwenda  kuzindua na kuhutubia Bunge Novemba 20, mwaka huu.
 
Umesema staili watakayoitumia ni tofauti na ile waliyoitumia wakati Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, alipozindua Bunge la 10 mwaka 2010 ya kutoka nje ya ukumbi kuonyesha kutotambua serikali yake. 

Akizungumza na mtandao huu katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma jana, aliyekuwa Mnadhimu wa Bunge la 10 Kambi la Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, alisema safari hii hawatatoka nje ya ukumbi wa Bunge  hata kama hawamkubali Rais Magufuli, kwa kuwa ni wajibu wao kushiriki vikao vya chombo hicho cha kuwakilisha wananchi.
 
“Sisi ni wabunge, tumo humu kwa ridhaa ya wananchi, tuna haki ya kuingia bungeni, hivyo siku hiyo tutaingia lakini kitakachotokea tutajua siku hiyo, bali haitakuwa kama walivyotuzoea tunatoka nje,” alisema na kuongeza:
 
“Subira yavuta heri, bado siku tatu tu, Watanzania watajua msimamo wetu tukiwa ndani ya Bunge nakuhakikishia lazima pachimbike,” alisema.

    Kuibuka huko kwa Tundu Lissu kuna kuja ikiwa ni baada ya taarifa kuzagaa mitandaoni zikisema ijumaa ya wiki hii Magufuli atalihutubia Bunge hili,huku inatajwa kuwepo na Rais aliyemaliza mda wake visiwani Zanziabr Dk Sheni jambo ambalo linatajwa ni uvunjavi wa katiba na kuna kwenda na  kinyume na utawala bora.
       Kwakuwa Ukomo wa Dk Sheni ulikoma rasmi tarehe 2 ya mwezi  huu kama katiba inavyomtaka kwihiyo kitendo cha kuwepo madarakani hakikubaliki na kinatafsiriwa ni sawa na udikteta.
      Kuzidi kukaaa huko madarakani kwa Dk sheni kunatokana na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi,Zanzibar ZEC,Jecha Salim Jecha kufuta uchaguzi wote visiwani humo bila ya kupewa mamlaka yeyoet ya Katiba,Uchaguzi huo ambao Jecha alifuta inelezwa kuwa mgombea wa chama cha wananchi CUF ambaye anaungwa mkono na UKAWA,Maalim Sefa sharif Hamad kuibuka ushindi wa nafasi ya Urais


Hivi karibuni aliyekuwa mgombea urais wa Ukawa kupitia Chadema, Edward Lowassa, alisema hawatambui matokeo yaliyotangazwa na Tume yaTaifa ya Uchaguzi (Nec) na kumpa ushindi Rais Magufuli na kwamba hawatashirikiana na serikali yake kutokana na kile alichoeleza kuwa uchaguzi mkuu uligubikwa na wizi wa kura na kuporwa ushind


No comments