Zinazobamba

SHEHE PONDA AIBWAGA SERIKALI MAHAKAMANI,APANGUA KESI ZOTE,SOMA HAPO KUJUA

ponda
 Mahakama ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia
Makosa yaliyokuwa yakimkabili ni mawili ambayo ni kushawishi watu kutenda kosa, pamoja na kutoa matamshi yanayoumiza imani ya dini nyingine.
Hakimu wa kesi hiyo Mary Moyo amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haukujitosheleza hivyo mahakama hiyo imemwachia huru na rufaa iko wazi endapo upande wa mashitaka hautaridhika na hukumu hiyo.
Shehe Ponda alikuwa anakabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo kushawishi wa imani wa dini ya Kiislam nchini kutenda makosa,ambayo anadaiwa kutenda kosa Ogost 2013,
Upande wa wa Serikali katika kesi hiyo uliwakilishwa na wakili wandamizi wa Serikali Berdard Kongola,Sunday Hrela na George Mbalasa wakati wa upande wa Mshtakiwa unawakilishwa Wakili Juma Nasoro ,Abubakal Salim na Bartholomeo Tarimo.

Awali kesi hiyo ilipangwa kutolewa hukumu 19 ya mwezi wa kumi ambapo shauri hilo lilihairishwa hadi Novemba 18 na kuhairishwa tena mpaka kutolewa hukumu hiyo leo,

Hakuna maoni