SAKATA LA KUWEPO VURUGU BUNGENI LEO,WANASHERIA WA LHRC WAMUANGUKIA SPIKA NDUGAI WASEMA AKIFANYA MCHEZO HUU ITAKULA KWAKE,SOMA HAPO KUJUA

NA KAROLI VINSENT
WANASHERIA kutoka kituo cha sheria na haki za
Binadamu (LHRC) wamemtaka Spika wa Bunge Job Ndugai kutomhuruhusu kuingia
Bungeni Dk Mohamed Shein na kutambulika kama Rais wa Zanzibar,
Badala yake wamemtaka kumruhusu kuingia kama
wageni wengine ili kuepuka vurugu.
Akizungumza na kituo cha Redio cha Magic Fm
katika kipindi cha Morning Magic,Mwanasheria wa (LHRC) Haron Sungusia amesema
ni wakati wa Rais John Magufuli atakapolihutubia Bunge ni vema Spika wa Bunge
akatumia busara ya kumtambulisha Dk Shein kama Mgeni rasmi kuliko Rais wa
Zanzibar.
“Namuomba Spika atumia busara ili aweze
kuliokoa Bunge kuingia kwenye fujo ni
vema akamtambulisha Shein kama mgeni tu wa kawaida maana suala la Zanzibar
sahivi lipo kwenye mgogoro mkubwa sana kutoka na uchaguzi kufutwa”amesema Sungusia
Sungusia
ameongeza kuwa Kikatiba ukomo wa Dk Shein kwenye nafasi yake ya Urais
kulishaishia tangu Novemba 2 mwaka huu ila hoja inayotumiwa kuwa ukomo wa Urais wa Shein
mpaka pale atakapohapishwa Rais mwengine haina mshiko kwa sasa kutoka na hali
ya kisiasa ilivyo.
Amebainisha
kuwa hata sheria za Zanzibar bado zinaonyesha kutokuwa na uharali wowote wa Dk
Shein kuwa Rais wa Zanziabr kutokana na Katiba kumbana.
Kuibuka
huko kwa Mwanasheria huyo kuzungumzia suala hilo,kuna kuja ikiwa ni teyari
wabunge wanaounda UKAWA wametishia kutomruhusu Rais Magufuli kulihutubia Bunge
bila suala la Zanzibarkutafutiwa ufumbuzi.
Akizungumza
na Fullhabari.blogs kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juzi,Mwanasheria mkuu
wa chama cha Demokrasia na Maendelea Chadema,Tundu Lissu amesema wao kama UKAWA
hawatakubali kwa mazingira yeyote yale Rais Magufuli kulihutubia Bunge.
Amesema
kwa sasa watatumia Mbinu tofauti na ile waliotumia mwaka 2010 walipomgomea Rais
mstaafu Jakaya Kikwete kwa kutoka nje ya Bunge ila sahivi wameapa kupambana
ndani ya Bunge huku wakificha stairi watakayoitumia kwa kuwataka watanzania
wasubiri waone.
No comments
Post a Comment