Zinazobamba

MAUZO KATIKA SOKO LA HISA YASHUKA KWA WIKI HII,SOMA HAPO KUJUA

Meneja Masoko wa DSE Patrick Mususa wakati wa mkutano na waandishi wa Habari akielezea hali ya mauzo katika soko la hisa
IDADI ya Mauzo katika soko la hisa mkoani Dar es Salaam,(DSE) kwa wiki hii yameshuka kwa asilimia  kwa asilima 55% hadi Bilioni 12.5 kutoka Bilioni 28 kwa wiki iliyopita.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
   Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam,Meneja Masoka wa DSE,Patrick Mususa amesema sababu iliyochangia kushuka kwa mauzo hayo inatoka na wawekazaji kupunguza hisa zao katika kaunta ya TBL.
     Mususa amesema pia  Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepungua kwa asilimia 19% pia hadi Milioni 1.7 kutoka Milioni 2.1 kwa wiki iliyopita.
       Hata hivyo Mususa amezitaja Kampuni tatu zilizoongoza kwa mauzo ya hisa ni .     CRDB kwa asilimia 47.88%2.     TBL kwa asilimia 44.86% pamoja na Benki ya      DCB kwa asilimia 2.86%
        Mususa amesema idadi ya mtaji katika soko imeongezeka kwa wastani kutoka Trilioni 21 hadi Trilioni 21.1 pamoja na Idadi ya mtaji wa makampuni ya ndani nayo imeongezeka kwa wastani kutoka Trilioni 9.7 hadi Trilioni 9.8,
Vilevile Mususa akawataka watanzani kuendelea kununua  hisa katika soko hilo kwa kupitia huduma ya kisasa ya simu kwa kupiga *150*36#


No comments