Zinazobamba

CHAMA KIPYA CHA SIASA CHAANZISHWA,SOMA HAPO KUJUA


MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AKIKABIDHI CHETI KWA MMOJA WA WAANZILISHI WA CHAMA KIPYA CHA TPF MASHUJAA.

MSAJILI  wa vyama vya Siasa nchini amekipa usajili chama kipya cha kisiasa cha  Tanzania Patriotic Front (TPF Mashujaa).Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo

Akitoa usajili huo leo jijini Dar es Salaam Mbele ya Wanahabari,Msajili wa Vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi amesema amekipa usajili wa mda chama hicho mpaka pale kitakapokamilisha sifa za usajili.

Amezitaja  Sifa hizo ni kupata idadi ya wanachama kutoka katika mikoa yote ya Tanzania bara pamoja na Visiwani.

Kwa upande wake Optatus Likwelile  ambaye ni mmoja wa waanzilishi wa chama hicho kipya, amewaambia wanahabari kuwa chama chake kitasimamia misingi ya haki ya umoja pamoja na kupambana na umasikini.

No comments