MALINZI AWAPONGEZA SAMATTA, ULIMWENGU

Katika
salamu zake kwenda kwa wachezaji hao, Malinzi amewapa hongera kwa
mafanikio waliyofikia ya kutwaa ubingwa huo wa vilabu Afrika, na
kuwataka waongeze bidii ili waweze kufanya vizuri pia katika michuano ya
Kombe la Dunia la Mabara litakalofanyika mwezi Disemba nchini Japan.
Malinzi
amesema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu na Watanzania wote
wanawashukuru kwa kuiwakilisha vizuri Tanzania kimataifa, na sasa moyo
huyo wa kujituma kwao waundeleleze katika mchezo dhidi ya Algeria
wikiendi hii kuwania kufuzu kwa fainali za kombe la Dunia 2018 nchini
Urusi.
No comments
Post a Comment