JUKATA WAMTAKA MAGUFULI KUGEUKIA KATIBA MPYA..
Jukwa
katiba nchini JUKATA limemtaka Rais mteule wa awamu ya tano wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Mh john Pombe Joseph magufuli kuendeleza mchakato wa
upatikanaji wa katiba mpya uliokuwa umesimama kutokana na shughuli za
uchaguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Mwenyekiti wa jukwaa
hilo Bw Deus Kibamba amesema kuwa mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya lazima
uendelezwe kutokana na kwamba ndo ilikuwa agenda ya kitaifa kabla ya taifa
halijaelekea kwenye uchaguzi.
Bw Kibamba amesema kuwa umuhimu wa kuwa na katiba
ya kisasa umejizihilisha wakati wa uchaguzi mkuu ambapo mambo mengi yamekiukwa
kutokana kukosa katiba inayoeleza mambo
katika misingi ya kuzingatia utawala bora.Aidha Bw Kibamba ameisihi
Bwana Deus Kibamba
amesema JUKATA wanamtaka Rais wa Tanzanaia Dr Magufuli baada ya kuzindua bunge
na kupata mawaziri wake ahakikishe kuwa kwanza analitangazia Taifa Rasmi namna ya
kurejea mchakato wa kupata katiba mpya,serikali ipeleke bungeni miswada ya
mabadiliko ya serikali zinazosimamia mchakato wa katiba,kurejea makubaliano ya Dodoma
ambayo yalitaka pia kupanua wigo wa wadau wahusika katika mchakato wa kupata
katiba ikiwemo pia nyama vya wafanyakazi,ambapo amesema kuwa kama rais atafanya
hayo anaweza kushinda mtihani wa serikali yake kuaminika na watanzania walio wengi.
Katika hatua nyingine
jukwaa la katiba nchini Tanzania JUKATA wamemtaka Rais wa Tanzania Dr Magufuli aweze kuongoza jitihada za kuinusuru Zanzibar kutumbukia kwenye mkwamo au
machafuko ya kisiasa hali ya sintofahamu iliyojitokeza baada ya uchaguzi ikiwa
ni pamoja na kutambua kuwa hatua ya umoja wa serikali ya kitaifa iliyokuwa
imeshafikiwa na wanzanzibar inapaswa kulindwa na kuheshimiwa.
Bwana KIBAMBA amesema
kuwa kwa mujibu wa waangalizi wa JUKATA waliokuwa wakiangalia uchaguzi wa Zanzibar
wameonyesha kuwa uchaguzi huo wa zanzibar ulifanyika na kumalizika kwa amani na
hakukuwa na dosari kubwa zilizokuwa zinaweza kuwafanya uchaguzi huo kuahirishwa
hivyo wameshangazwa sana hatua ya mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar Kufuta
uchaguzi huo.
No comments
Post a Comment