Zinazobamba

RAIS KIKWETE LAWAMANI TENA,APEWA SAA 48 ZA MWISHO ZANZIBAR,SASA NI KUSUKA AU KUONYOA,SOMA HAPO KUJUA

Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad
Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad

RAIS Jakaya Kikwete ameingia kwenye lawama nzito baada  ya kutuhumiwa kutumia madaraka yake kutaka kumpokonya ushindi Mgombea wa Urais kupitia chama cha wananchi CUF ambaye anaungwa mkono na vyama vya UKAWA,Maalim Sef Sharif Hamaad.Mtandao huu unaripoti.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
      Taarifa kutoka Dar es Salaam na Visiwani Zanzibar zinasema kitendo cha mwenyekiti wa wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) bwana  Jecha Salim Jesha kufuta uchaguzi wote na kutangaza kufanyika tena ndani ya siku 90 kwa kile anachokisema uchaguzi huo ulikuwa na kasoro lukuki,kumeingiza idara ya Rais kwenye kashfa.
      Kwani Kitendo hicho cha Jesha kufuta uchaguzi huo kinakwenda na kinyume na sheria za nchi kutokana na Mwenyekiti huyo kutokuwa na mamlaka yeyote ya kisheria ya kufuta uchaguzi huo ambao inadaiwa mgombea wa CUF alikuwa ameshinda nafasi ya Urais ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya kumwacha kwa mbali mpinzani wake Dk Mohamed Sheni.
      Kwa mujibu wa mtoa taarifa wetu aliyoko ndani ya ZEC ameumbia mtandao huu kuwa,kitendo alichokifanya Jecha cha kufuta uchaguzi huo umetokana na yeye mwenyewe huku akidaiwa kushinikizwa na kigogo mmoja wa juu wa chama cha Mapinduzi CCM.
     “Ujue hapa tunapoelekea lazima damu itamwagike,maana leo viongozi wote akiwemo Dk Sheni,Rais Kikwete wamekaa kimya wana mwacha Jesha anafuta uchaguzi pasipo hata kumkemea, huko wote tukifahamu kuwa hakuna kipengele chechote cha Katiba kinachompa mamlaka hayo Jesha,”
      Amesema wao wanamtuhumu Rais Kikwete kuhusika kwake inatokana na yeye kunyamazia au naye kuhusika kwa moja kwa moja kutokana na kitendo cha kumfumbia macho Mwenyekiti huyo wa ZEC kuvunja katiba ya nchi kwa kufuta uchaguzi huo,
Amesema Idara ya Urais ni ingetakiwa kusimamia na kuilinda katiba ya Jamhuri ya Muungano lakini cha ajabu hakuna hata kalipio kutoka wa Rais Kikwete kwa mwenyekiti huyo Jambo linalotia shaka uwenda nayo idara ya Rais inahusika.
     Kuibuka kwa tuhuma hizi kwenye Idara ya Ikulu, kunakuja ikiwa ni siku moja baada ya Mwenyekiti wa kamati ya Uongozi ya CUF,Twaha Issa Taslima kuibuka na kusema kwamwe chama chake akitashirikia kwenye uchaguzi mwengine kutokana na mwenyekiti wa ZEC kutokuwa na mamlaka kamili ya kufuta uchaguzi.
      Akizungumza na waandishi wa habari jana,Taslima amesema jambo linaloshangaza ni kuona mwenyekiti wa ZEC kutangaza kufuta uchaguzi bila ya kuwashirikisha makamishna wake,
     “Hili linathibitishwa na taarifa ya vyombo vya habari iliyotolewa na makamishna wa zec kukanusha kuhusika na uamuzi huo wa mwenyekiti wa zec,ambapo hatua hii ni uvunjwaji wa katiba ya Zanzibar (1984) ibara ya 119(10)  inayotaka vikao vya ZEC kuhudhuriwa na mweyekiti na makamu mwenyekiti na wajumbe wane4 na uaamuzi kuungwa mkono na walio wengi”amesema Taslima.
  Kuibukua huko kwa CUF kunakuja ikiwa ni teyari mataifa ya Ulaya,yakiwa yakikipinga kitendo cha ZEC kufuta uchaguzi nao wao wakiishinikiza ZEC kumalizia kutangaza matokeo hayo huku wakisema hakuna dosari yoyote iliyojitokeza kwenye uchaguzu huo kwani uchaguzi wote ulifanyika kwa uhuru na haki.
     Mbali na ZEC kufuta uchaguzi wa Zanzibar kunazidi ibua mashaka baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.NEC,Jaji Mstaafu Damian Lubuva  kulipinga jambo hilo na kusema ZEC haina mamlaka ya kufuta uchaguzi huo,
 Sanjari na Lubuva,naye Mwanasheria mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Tundu Lissu ameishukuia ZEC kwa kusema haina mamlaka hayo kisheria huku akiwataka Wazanzibar kudai haki yao barabarani.
     Mjadala huu,unafunga na Maalim Sef mwenyewe baada ya kutoa saa 24,ZEC iwe imemtangaza mshindi badara yake atawaachia Wazanzibar wenyewe waamue,
Amesema amefanya jitihada za kutosha kutaka kulimaliza suala hili,ila imeshindikana baada ya kumpigia simu Rais Kikwete pamoja Rais Sheni huko wote kwa pamoja simu zao kutopokelewa.

Amesema machafuko yakitokea asije akaja kulaumiwa mtu

No comments