Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO,.KUMEKUCHA URAIS CCM, YALIYONENWA SASA WAZI WAZI,JAJI AGUSTINO AJITOSA ,MITETEMEKO KUNYWEA SOMA HAPO KUJUA


pichani ni Jaji Ramadhani akichukua fomuya Urais leo Mkoni Dodoma
akiongozana na Mkewe
HATIMAYE makundi hatari ndani ya chama cha Mapinduzi CCM yaliyojitokeza kutokana na Makada wake wanaotaka Urais kwenye chama hicho yamepatiwa dawa,baada ya Jaji Agustino Ramadhani kujitokeza na kuchukua fomu ya Urais  .Mtandao huu umedokezwa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
          Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umepenyezewa kutoka ndani ya Chama hicho kikongwe zinasema kuibuka kwa Jaji Ramadhani kutajwa kuwa ni mwarubaini kwa makada wa Chama hicho waliojiapiza kufa na CCM endapo watakatwa majina yao.
       Makada hao wakiongozwa na Waziri mkuu aliyejiuzulu kwenye Kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni ya Tata ya Richmound Edward Lowassa ambapo mara kwa mara amekuwa akijiipiza kwa kupitia marafiki zake akisema ni “Bora CCM imeguke kuriko yeye kukosa Urais mwaka huu”.
          Jaji Agustino Ramadhani amechukua Fomu hiyo ya Urais leo Mkoani Dodoma huku akijinasibu kukuza uchumi wa Tanzania na  kutatua  tatizo la Ajira anatajwa viongozi wandamizi wa Chama hicho kuwa ndio itakuwa mwisho na Makundi yanayotajwa kukitesa chama hicho na kupelekea kudhohofika .
     “Hapa makundi ndio basi tena teyali tumeyazima nakwambia huyu hana mpinzani kwa hao mafisadi wanaohonga pesa kwa watu, maana chama chetu kinambinu hatuwezi kupelekeshwa na mafisadi wachache,wakati chama hichi chenye viongozi wengi na waaminifu kwa jamii”amesema Kiongozi Mmoja wa CCM kwa sharti la kutatajwa jina lake mtandaoni.
         Sifa ambayo inatwajwa na CCM kwamba Jaji huyo ambaye alikuwa Luteni Kanali ndani ya Jeshi la Wananchi (JWTZ)kwenye miaka 1978 inaelezwa kwamba ni mzaliwa kutoka Visiwani Zanzibar ,tena anaelezwa pia hana Kashfa ya Ufisadi inayomkabili ambayo haitawapa kazi kumnadi kwenye Kampeni endapo Jina lake likipita.
      “Sikiliza kwa sasa hali muungano imekuwa mbaya sana maana hata wewe shahidi kwahiyo kuingia Jaji Ramadhani kutarudisha Hadhi ya Muungano ambayo ilipotea kwa mda mrefu na pia huyo mtu ni mchapa kazi sana”
      Ameongeza kuwa kwa kusema “harafu huyu sio hao wengine wamechafuka sana kwenye Kashfa kubwa za Ufisadi unategemea CCM ni wajinga sana wamteue mtu kama huyo harafu tuwape upenyo UKAWA,maana miaka ya leo vyama vya Upinzania vimekuwa sana na CCM hatuwezi kufanya Makosa”  
     HISTORIA YAKE
     
        Taarifa zake zinaonyesha kuwa pia amesoma  shule mbalimbali za msingi Mpwapwa mkoani Dodoma 1952 -1953 nikaenda Town School-Tabora na pia akasoma darasa la tatu hadi la nne mwaka 1954-1956 na darasa la sita na saba na akasoma  KazelHill ambayo kwa sasa inatwa Shule ya Msingi Itetemia mwaka 1957-1958. Na darasa la nane tu mwaka 1959 na akarudi kusoma Mpwawa.
       Pia, Mwaka 1960-1965 alijiunga na Tabora School kwa ajili ya masomo ya kidato cha kwanza hadi cha sita. Pai  akafaulu na kuchjaguliwa kujiunga
 na kuchkua  shahada  ya Sheria na ilipofika Machi 1970 na kuhitimu elimu yake hiyo.



   Taarifa hiyo inaelezwa kuwa mwishoni mwa Machi wa mwaka huo huo wa 1970 akajiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), na kuingia  jeshini kama mwanasheria raia mpaka kipindi cha mafunzo ya kijeshi akaenda kwenye mafunzo
na baada akarudi kuitumikia JWTZ.
    Na lipofika mwaka 1971 akapewa kamisheni kambi
ya Mgulani akiwa Luteni (nyota mbili). Na kuendelea na jeshi hadi mwaka 1977, nakuhamishiwa na Brigedi ya Faru-Tabora nikiwa na cheo cha Meja.

         Taarifa za Jaji huyo kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Urais ndani ya CCM hiyo ziliibuliwa na Magazeti yanayotoka mara moja kwa wiki ambayo ni Gazeti Mawio na Raia Mwema pia vilevile mwaka 1978, ,  rais wa  Zanzibar na akumteua kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar na
kipindi hicho Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwani Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Damian Lubuva.


      Aidha, Oktoba 1978 akateuliwa  kuwa Jaji Mkuu
wa Zanzibar. Na ilipofika Machi 1979 alirudishwa JWTZ na baada ya muda mfupi  akapelekwa kwenye vita ya Uganda , na kupewa cheo  cha Luteni Kanali na kwenye vita hiyo alikuwa anaendesha mahakama za kijeshi
.
   Vilevile baada ya Vita ilipokwisha akarudi zake Zanzibar. NaJanuari 8 mwaka 1980 akaapishwa kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar, wakati huo akiwa na cheo
cha Luteni Kanali. Huku akiendelea na Ujaji Mkuu Zanzibar hadi Septemba 1989
alipoapishwa Jaji Mkuu Zanzibar Hamid Mahamod Hamid.

       Hata hivyo Juni 23 mwaka 1989 aleteuliwa kuwa
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania hadi mapema wiki hiyo alivyoteuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Chanzo cha FULLHABARI.BLOG kinaoenyesha kuwa aliteuliwa  kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani
hapa Bara ndiyo sababu ya kuacha ujaji Mkuu Zanzibar.


      Januari 1993 akateuliwa kuwa Makamu
Mwenyekiti katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kuendelea nayo na nafasi hiyo
hadi Januari 2003 na Oktoba 2002 mpaka alipoteuliwa  kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ambapo kipindi c cha miaka mitano katika
tume ZEC kinamalizika Oktoba mwaka huu

         Novemba 2001, aliteuliwa kuwa Jaji wa
Mahakama ya Afrika Mashariki nafasi ambayo alitakiwa kumaliza  kipindi  cha
miaka sita Novemba mwaka huu.

      KUHUSU NDOA
     Jaji huyo mwenye aiba ya upore anamke mmoja ambaye Mungu amebahatik kupata watoto wanne, wawili ni wasichana na wawili ni wavulana.
     Mtoto wake wa kwanza anaitwa Francis (30)
huyu ni mwanasheria na anafanyakazi ya uwakili Manchester, Uingereza, Brigeth,
huyu ana shahada ya Uandishi wa Habari na anafanyakazi ICAP hapa nchini, Marina
ni mfamasia, yuko Liverpool, Uingereza na Mathew naye ni mfamasia, anafanya
kazi Liverpool.”



No comments