HABARI KUBWA LEO,KIKWETE AACHWA "MTUPU" NA WATIA NIA YA URAIS,WENGI WAJIGEUZA WAPINZANI WAISHAMBULIA SERIKALI YAKE ,SOMA HAPO KUJUA
pichani ni Rais Kikwete |
MAKADA wa
chama cha Mapinduzi CCM waliotangaza nia za kutaka Urais ndani ya Chama hicho
kwenye Uchaguzi Mkuu wa hapo baadae mwaka huu,wamemuweka “mtupu kama asiyekuwa
na nguo” Rais Jakaya Kikwete.mtandao huu
unaweza Kuripoti,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Makada hao ambao asilimia kubwa
walikuwepo kwenye Utawala wa Rais Kikwete,wameonesha wazi kwamba kama hawakuwa nchini,kutokana na kuweka sera zao wakati walitakiwa hata kuzitelekeza wakati wakiwa kwenye Uongozi.
Miongozi mwa makada hao ni Waziri mkuu
aliyejiuzulu kwenye kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound , Edward
lowassa ambaye aliwaambia watu wanaojiita “Jukwaa la Wahariri” wiki mbili
zilizopita na kuponda sera ya Kilimo kwanza na kusema Elimu ndio ingetakiwa
kuwa kipaumbele.
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli ni
miongoni mwa watu waliitengeneza Ilani ya CCM mwaka 2005 wakati wa Rais Kikwete
anaingia madarakani ,ambayo sera ya kilimo kwanza ndio ilikuwa miongoni mwa
Ilani hiyo.
Mbali na Lowassa makada wengine walioivua
“nguo” Serikali ya Rais Kikwete ni Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba ambaye
naye wakati akitangaza nia ya kutaka Urais ndai ya chama hicho kinachozeekea
madarakani kwa kusema atapambana kuinua uchumi wa nchi huku akisema tangu apata
Unaibu Waziri ameshudia misamaa ya kodi kwa matajiri.
Mwigulu
ambaye alikuwa Naibu Katibu mkuu Bara CCM,ameonyesha kuwashangaza watu kwakuwa
yeye alikuwa miongoni mwa Baraza la Mawaziri la Serikali ya Kikwete ambao kila
jambo ambalo Serikali wanaamua lazima likubalike na baraza hilo lakini
ameshindwa kupambana na suala hilo .
Sanjari na Mwigulu Nchemba makada
wengine walioiweka Rehani CCM ni Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Steven
Wassira ambaye naye alikemea Ufisadi ambayo chama chake kwa kiasi Kikubwa
kimechangia kuleta Ufisadi huo.
Naye Pia Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta
naye wakati anatangaza nia Jimboni kwake alisema atahakikisha kudumisha
muungano na kupambana na Rushwa na Ufisadi, wakati Sitta huyo ndio alikuwa
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba ambalo kwa kiasi Kikubwa “lilizika” maoni
ya Wananchi yaliyowabana wala Rushwa.
Akizungumza na Mtandao huu Mjumbe wa
Halmashauri kuu ya CCM kutoka Mkoani Morogoro amesema kwa sasa CCM inavuliwa
nguo.
“Mimi nashangaa sana,hawa wote tu
walikuwa kwenye utawala huu ambao Rushwa imekuwa kubwa,tena watuhumiwa wa
Ufisadi wameachwa,harafu leo wanakuja kutuambia kwamba watapambana na Rushwa
huu ni utoto tu wanamuabisha Mwenyekiti wetu”amesema mjumbe huyo
“Hawa watu
wakati wakichangia Bungeni wanasema Serikali ya CCM,imefanya Makubwa,huku
Serikali hiyo hiyo imekumbatia watu walioifilisi nchi kwenye Mikataba ya
Richmound,mimi nawaomba watanzania tuwe makini jamani”amesema Wananchi wa
kawaida.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni