Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-RAFU MBAYA YA PINDA,AFUJA KODI ZA WATANZANIA KWENYE URAIS WAKE,SOMA HAPO KUJUA



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma
   



ANAYEJIITA na Kuitwa mtoto wa Mkulima,Waziri mkuu Mizengo Pinda imebainika anatumia Pesa za walipa kodi katika harakati zake za kutaka Urais ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM,(Mtandao huu unafahamu),Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
      Waziri mkuu Pinda ambaye ni miongoni mwa Makada wa CCM walitangaza nia ikiwemo kuchukua Fomu na kwa sasa yupo mikoani mbali mbali akitafuta wadhamini 450 Katika Mikoa 15 ya Tanzania Bara na Visiwani.
        Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu wa Mtandao huu aliyoko kwenye Ziara ya Pinda kusaka Wadhamini ameupasha mtandao huu kwamba Kiongozi huyo amekuwa akitumia mafuta ya Serikali,Mgari ya Serikali pamoja na Watumishi wa Serikali.
        “Yaani kinachofanyika huku ndugu yangu ni kama kazi ya kusaka Wadhamini imekuwa ya Serikali hapa Kodi ya Serikali inatumika,kughalamia mafuta,kuwalipa madereva hawa mpaka mtu unajiuliza hivi anafanya hivi kwa misingi ipi wakati mambo ya chama haya husiani na Serikali?”amehoji
     Mbali na kutumia Mafuta yanayotokana na Serikali pia Waziri mkuu Pinda anatuhumiwa pia kuongozana na Kitengo cha Habari kilichopo Wizarani kwake.
“Tena ameongozana na Waandishi wa Habari wa Serikali,ambao wote wanalipwa kutokana na Kodi zetu mpaka unajiuliza hivi anachafanya akikubaliki kabisa hawa ni watumishi wa Umma sahivi wangetakiwa wawe wanafanya kazi za kusaidia umma,sasa anavyowatumia kuwatafuta wadhamini ni kosa la Jinai na kukiuka Katiba ya nchi”
    Pinda,ambaye kwenye utawala wake anatuhumiwa kufumbia macho Uporaji wa Mabilioni ya Shilingi kwenye Akaunt ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu pamoja na kutuwashughulikia watendaji wa Mkoa wa Dar es Salaam waliuza Shirika la Usafiri la UDA kifisadi, pia anatajwa kutumia wakurugenzi mbali mbali wa Halmashauri kumsaidi kumtafutia wadhamini.

No comments