EXCLUSIVE-PROFESA LIPUMBA AMLIPUA LOWASSA,KINGUNGE,AMTAKA HOSEA WA TAKUKURU KUMCHUNGUZA LOWASSA MARA MOJA SOMA HAPO KUJUA
Pichani ni Profesa Lipumba akizungumza jambo na wandishi wa Habari picha na maktaba |
MWENYEKITI
wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba ni kama amemshukia Edward
Lowassa ambaye ni miongoni mwa Makada wa Chama cha Mapinduzi CCM ambao
wanautaka urais kwa Udi na Uvumba kwa kusema ni Mtu hatari ambaye watanzania
wanatakiwa kumwogopa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Vilevile Profesa Lipumba amemshukia pia
Mwanasiasa Mkongwe nchini Kingunge Kombale Mwiru na kusema amemsaliti Mwalimu
Julias Nyerere kwa kuwashabikia watu mafisadi.
Hayo yamesemwa na Profesa Lipumba leo
Jijini Dar es Salaam Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo Profesa
lipumba amemtaka Mkurugenzi wa TAKUKURU Edward Hosea kumchunguza mara moja
Edward Lowassa kwa hatua yake ya awali aliyotangaza nia kwa kusema ametumia
pesa nyingi huku akionyesha wazi yeye ni mtumishi wa umma.
“Mimi nashangaa sana ofisi ya Hosea kuwa
kimya kwa watu kama wakina Lowassa,ambao kutangaza nia tu wametumia ghalama
kubwa huko tunajua wazi hawa ni watumishi wa Umma wasiku nyingi pesa hizi
wanazitoa wapi za kukodi mamia ya watu toka mikoa mbalimbali na kuwalipa posho
kubwa sana, sasa huyu mtu pesa katoa wapi na atazirudishaje?watanzania wawe
makini sana”amesema Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba ameongeza kuwa kwa kusema hata Watangaza nia ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM
kutumia pesa nyingi imeonyesha wazi kwamba walifanya makusudi “kunyofoa”Maoni ya Wananchi kwenye Katiba pendekezwa ambayo iliwabana watumishi wa Umma kutangaza
mali zao zote.
“Hawa wakina lowassa pamoja na wenzake
walitumia nguvu kubwa kuzika maoni ya wananchi kwenye katiba ile husasani
kwenye kipengele ambacho kinawataka Viongozi kutangaza mali zao pamoja na pesa wanazomiliki kabla ya kuwania sehemu mbali
mbali za uongozi,kumbe walikuwa
wanamalengo haya”ambainisha Profesa lipumba.
KUHUSU SUALA LA KINGUNGE.
Profesa
Lipumba ambaye ni Gwiji wa masuala ya uchumi Dunia ameonyesha masikitiko yake kwa
Mwanasiasa Mkongwe kutokana ndani ya CCM kingunge Kumbale Mwiru kitendo chake cha kwenda
Arusha kwenye Mkutano wa Hadhala uliondaliwa na Edward Lowassa wenye ajenda ya
kutangaza safari ya matumaini.
Ambapo
Lipumba amesema Mwanasiasa huyo amemuongusha Mwalimu Nyerere ambaye ni mtu
mtetezi wa Masikini.
“Hivi naweza
kusema Mzee mwezangu Kingunge hizi ni njaa au sijui ?maana namjua Kingunge
huyo kwenye miaka ya 1970 alikuwa anakuja na kunadi Sera za Ujamaa na
kujitegemea,hivi hizi sera za kuwa upande wa Mafisadi ni ndio Ujamaa wa Karne
ya 21 ua?”amehoji Profesa Lipumba.
Katika hatua
nyingine Chama hicho cha CUF ambacho kinaunda Umoja wa Vyama vinavyounda UKAWA wameipongeza Tume ya Haki za Binadamu na Utalawa Bora ambayo ilitoa Ripoti
kuhusu tukio lilitokea Januari mwaka huu kwa wafuasi wa Chama hicho ambao walikuwa
wakienzi kumbukumbu ya Miaka 16 ya kifo cha Wananchama wake kiliochotokea 2001
Visiwani Zanzibar.
Ambapo kwa mujibu wa Ripoti hiyi ilionyesha
Jeshi la Polisi kutumia nguvu kubwa kuwapiga wananchama hicho huku ikivunja
kanuni za Vyama vya Siasa nchini,kwa mujibu wa Lipumba anasema Ripoti hiyo
wao wameipokea kwa moyo mmoja na
wameitaka Serikali kufanyika kazi mapendekezo yake.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni