Zinazobamba

SHIRIKA LA THE SAVE CHILDREN LAWAKUTANISHA WANASIASA NA WATOTO,WASEMA MENGI SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Meneja Mwandamizi wa Shirika lisilo la Kiserikali linalohusika na Mambo ya watoto nchini la ‘The Save children’  bwana Mussa Mugita
akizungumza na
waandishi wa Habari

WITO umetolewa kwa Vyama vya Siasa nchini kuweka kipengele cha Watoto kwenye Ilani zao za Uchaguzi unaotarajia kufanyika hapo baadae mwaka huu kwa kusema ndio itakuwa njia ya kumkomboa Mtoto wa kitanzania anayetazamwa kama ametengwa na Vyama hivyo vya Siasa nchini.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
    Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Meneja Mwandamizi wa Shirika lisilo la Kiserikali linalohusika na Mambo ya watoto nchini la ‘The Save children’  bwana Mussa Mugita wakati wa Semina iliyowakutanisha Viongozi mbali mbali wa Vyama vya siasa nchini pamoja na Baraza la Watoto lenye lengo la kujadili changamoto mbali mbali zinazowakumba.
Ambapo Bwana Mugita amesema kwa sasa mtoto wa kitanzania ni kama amesahulika na vyama vya siasa katika ilani za uchaguzi jambo ambalo anadai kuwa limechangia kuteseka kwa mtoto wa kitanzania na kumfanya akose mahitaji ya Muhimu.
Kwa mujibu wa Meneja huyo amesema nia ya Shirika hilo ni kurudisha matumaini kwa mtoto wa kitanzania ambaye amekuwa akitengwa na wanasiasa hayo kwa kuwakutanisha na Viongozi mbali mbali wa Siasa wenye Jukumu la kutengeneza Ilani zao kwenye Vyama vyao vya Kisiasa.
Kwa upande wao Viongozi mbali mbali vya Vyama vya Siasa walihudhulia Semina hiyo walitoa masikitiko yao kwa Serikali iliyopo Madarakani ambayo ni chama cha Mapinduzi CCM kwa kuwatenga watoto kitanzania kwa kushindwa kuwapa Elimu bora pamoja na Ulinzi jambo ambalo wanazidi dai limewakatisha tamaa watoto.


         Wanasiasa huo ni Peter Mzirahi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini,Lilian  Bendera ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Chama cha NDC wate kwa pamoja waliitupia lawama Serikali nchini kwa kuwatenga watoto.


Hakuna maoni