WAMILIKI WA MABASI WAIANGUKIA SUMATRA,PIA WAFICHUA SIRI ZA SABABU YA AJALI,SOMA HAPA KUJUA

CHAMA cha Wamiliki wa Mabasi nchini (TABOA) wameitaka Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kuwapa miezi mitatu ya Majaribio ili kutekeleza Azamio la
Mamlaka hiyo linalowataka wamiliki hao kuwaajiri madereva wawili kwenye mabasi
yanayokwenda masafa marefu.Anaripoti KAROLI VINSENT endelea nayo
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es
Salaam na Mwenyekiti wa (TABOA)Elenea Mrutu wakati wa mkutano mkuu wa Dharula
uliowakutanisha wamiliki mbali mbali wa Mabasi wenye lengo la kujadili wimbi la
uongezeko la Ajali linaloongezeka kila kukicha nchini.
Ambapo amesema nia ya Serikali na
Sumatra kuwataka wamiliki hao kuwa na utaratibu wa madereva wawili ni nzuri ila
wanaitaka mamlaka hiyo kutoa miezi mitatu ya maribio ili kuweza kujua umuhimu
wake na kujiweka utayari wa kutekeleza azimio hilo.
Bwana Mrutu ameongeza kuwa kwa sasa
Mfumo wa sasa wa kuwa na Dereva mmoja umesababisha madereva kuchoka na
kupelekea kutokea kwa ajali ambapo amedai mfumo huu wa sasa wa kuwa na Madereva
wawili utasaidia kuondoa Tatizo hilo ambalo limegalimu vifo vya Watanzania.
Kwa upande wa Wamiliki wa mbalimbali
wa Mabasi wameitupia lawama serikali kwa kushindwa kutekeleza matakwa yao
ambayo walikuwa wanaitaka serikali kuongeza mda wa usafirishaji toka mda wa
sasa wa saa kumi na mbili hadi masaa 24 jambo ambalo wanadai kufanya hivyo
kutaweza kuwafanya madereva kupunguza mwendo kasi.
Sanjari na hilo Wamiliki hao wamelalamikia
pia Ubovu wa Miundombinu ikiwemo Barabara na msongamo usio na lazima ambapo
bwana Emmanuel Sawaya Mmiliki wa Basi la Kilimanjaro Express anadai
limesababisha Janga la Ajari nchini.
No comments
Post a Comment