BREAKING NEWS,NI MGOMO MWENGINE TENA WA MABASI,KUANZA RASMI ALHAMISI,WASEMA LIWALO NA LIWE,SOMA HAPA KUJUA
WAMILIKI wa
Mabasi yaendayo mikoani nchini (TABOA)
wameitangazia mgomo wa Mamlaka ya Usafirishaji wa Majini na nchi Kavu (SUMATRA)
kuhusu nauli mpya za mabasi zilizotangazwa na Mamlaka hiyo kwa mabasi yanayoenda
Masafa marefu ambazo nauli hizo zilitarajiwa kutekelezwa kwake Alhamisi ya wiki
hii kwa kusema hawataruhusu mabasi yao kupakia Abiria .Anaripoti KAROLI VINSENT
endelea nayo.
Akitangaza Uamuzi huo wa Mgomo leo Jijini Dar es Salaam na Katibu mkuu wa TABOA
Bwana Erenea Mrutu wakati wa Mkutano wa
Dharula uliowakutani Wamiliki mbali mbali wa Mabasi wenye lengo kujadili
auamuzi wa Sumatra kuhusu nauli hizo mpya pamoja na ongezeko la Ajali ambapo
amesema kwa sasa TABAO wamefikia uamuzi huo kutokana na Sumatra kutofuata hali halisi ya Garama za usafirishaji pamoja na
kushuka kwa shilingi ya Tanzania pamoja na ongezeko la Mafuta kwenye Soko la Dunia
ambapo inaonyesha mafuta kupanda kila kukicha.
Pamoja na hayo amebainisha kuwa kwa
Wamiliki wa Mabasi wanafanya biashara anaodai ni ya Hasara kutokana na Mafuta
kuwa juu na kitendo cha wao kuendelea kufanya biashara ya kupakia Abiria ni kufanya kazi anaodai ni ya Hasara,ambapo anasema Jambo ambalo Sumatra wanashindwa kulitambua na kuendelea
kupunguza Nauli za Mabasi.
Kwa upande wao Wamiliki wa Mabasi wameitupia Lawama SUMATRA kwa kusema inawadharau wamiliki hao kwa kuwachukulia watu wa kawaida.
“hatutakubali
kabisa,hawa watu hawana huruma na maana mimi leo nimewekeza zaidi ya Bilioni 9
kwenye ununuzi wa magari lakini wanatupuuza na tunajua lengo la kufanya hivi
tufilisike na kazi hii ili wawape watu wao kutoka China tunasema hatukubali na
iyo tarehe 29 hatutoa mabasi yetu na wafanye wao kazi maana hii biashara ni
hasara tu, mbona wao serikali wameshindwa wanataka na sisi kwamba tufulisike
hatukubali”
ENDELEA KUFUATILIA MTANDAO HUU UTAPATA TAARIFA KAMILI KWANI MWANDISHI WA MTANDAO HUU KAROLI VINSENT YUPO KWENYE MKUTANO HUO WA TABOA
ENDELEA KUFUATILIA MTANDAO HUU UTAPATA TAARIFA KAMILI KWANI MWANDISHI WA MTANDAO HUU KAROLI VINSENT YUPO KWENYE MKUTANO HUO WA TABOA
Post Comment
No comments
Post a Comment