Zinazobamba

HABARI KUBWA-VIDAGAA WENGINE WA ESCROW WAPANDISHWA MAHAKAMANI,RUGIMALIRA AZIDI KUWAPONZA SOMA KUJUA


NA KAROLI VINSENT
SIKU moja kupita baada ya Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kuwapandisha washtakiwa wawili kwenye mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam   kwa tuhuma za kupokea Rushwa kutoka kwa Mkurugenzi wa VIP Engineering bwana James Rugimalira ambapo pesa hizo ni za Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu (BOT).
      Hatimaye tena leo  Taasisi hiyo ya kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imewapandisha  watendaji wengine wa serikali kwa kosa ya kupokea Rushwa zenye Thamani ya zaidi ya Bilioni 2.6 za kitanzania kutoka kwa mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering bwana James Rugimalira ambazo pia ni pesa za Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa BOT.
     Wakisomewa Mashtaka yao kwa nyakati Tofauti kwenye Mahakama ya hakimu mkazi kisutu watuhumiwa hao Mwanasheria mwandamizi wa Shirika la Umeme nchini TANESCO Steven Urassa  akisomewa shtaka lake Mwanasheri wa TAKUKURU  Bwana Leonard Swai mbele ya hakimu Devota Kisila ambao ilidaiwa mtuhiwa alipokea Rushwa kutoka kwa Bwana James Rugimalira kupitia Akaunti ya Bank ya Mkombozi milioni 194 huku akijua anafanya kosa.
       Mwengine ni Kyabukoba leonald Mutigwa ambaye naye ni Meneja wa Kodi kutoka  Mamlaka ya kodi nchini (TRA) ambapo pia alisomewa shtaka na Mwanasheria wa TAKUKURU bwana Leonald Urassa anadaiwa kupokea Rushwa ya milioni 191 kutoka kwa mkurugenzi wa VIP Engineering Bwana James Rugimalira kupita Akaunt ya Banki ya Mkombozi.
 Vilevile mwengine pia ni Julius Rutta mkurugenzi wa Benki Kuu nchini (BOT) naye alifikishwa makamani hapo na kusomewa shtaka lake na Bwana Leonald Swai  mbele ya Hakimu Janeth Kalugenda ambapo anatuhiwa na TAKUKURU  kupokea Rushwa ya Milioni 382 pamoja na Bilioni 1 kutoka kwa Mkurugenzi wa VIP Engineering bwana  James Rugimalira huku akijua ni kosa.

Kati ya watuhuiwa watatu Mtuhumiwa mmoja tu Bwana Steven Urassa ndio aliyekizi vigezo vya Dhamana na sasa yuko nje lakini wengine wameendelea kusota Rumande.

ENDELEA KUFUATILIA MTANDAO HUU UTAPATA ZAIDI KWA UREFU

Hakuna maoni