Zinazobamba

HABARI KUBWA-GAZETI LA MWANANCHI LABOMOLEWA TENA,MHARIRI WAKE MWENGINE ACHUKULIWA,NI MUNDELEZO WA KUKIMBIWA SOMA HAPA KUJUA

pichani ni Neville Meena picha na Maktaba
NA KAROLI VINSENT
ZIMWI la kukimbwiwa na Waharri pamoja na Waandishi wake bora lazidi kulitesa Gazeti la Mwananchi baada ya hivi sasa Mhariri wake Mwingine ambaye  pia ni Msimamizi wa dawati la Habari za Uchunguzi  Neville Meena naye amelikimbia Gazeti hilo na kuhamia  Gazeti la kila siku la Tanzania Daima.MTANDAO huu umedeokezwa.
       Kuhama huko kwa Neville Meena kumekuja ikiwa miezi michache kupita baada ya aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti  la Mwananchi Tido Mhando kuhamia Kampuni ya Azam media.
       Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata zinasema Neville Meena amehamia rasmi Gazeti la Tanzania Daima na kupewa nafasi ya Mhariri Mtendaji.
     Nafasi ya mhariri mtendaji kwenye Gazeti hilo  hapo awali ilikuwa inashikiriwa na Asbert Ngurumo ambaye sasa amejiingiza katika masula ya siasa ambapo anatarajiwa kugombea Ubunge kwenye Jimbo moja katika mikoa ya Kanda ya ziwa.
            Neville Meena ambaye ni katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEC) kuja kwake kwenye gazeti la Tanzania Daima kunatajwa na wachambuzi wa Masuala ya habari ni kuzidi kuleta mapinduzi katika Gazeti hilo bora kwa sasa nchini ambalo mara kwa mra limekuwa likimbumbana vikwanzo na Serikali kutokana na kuchapisha habari Zenye kuihuzi idara mbalimbali za Umma ambazo hazitaki kuambiwa ukweli.
        Hii si mara ya Kwanza kwa Gazeti la mwananchi kuzidi kukimbiwa na Wafanyakazi kwani kipindi cha Miaka miwili iliyopita iliwai kukimbia na Wahariri wake ,waandishi pamoja wasambazaji wa Gazeti hilo.
       Wahariri hao ni Dennicy Msack ambaye nae alikacha gazeti hilo na kumbilia kwenye Kampuni ya  Newhabari ambao ni wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania,The African,Rai Nguvu ya Hoja,Bingwa pamoja Dimba.
         Mbali na Msack wengine waliokimbilia Kampuni ya NewHabari ni Edwin Mjahuzi ambaye alikuwa mpiga picha mkuu anatajwa kuwa alikuwa kiungo muhimu kwenye gazeti la Mwananchi na mhariri wa Habari wa Habari Samsoni Mfalila.
        Si wahariri pamoja na wasambazaji tu peke yake waliokimbia katika Gazeti la Mwananchi na hata wapiga picha walikimbia Gazeti hilo na kwenda katika Gazeti la Mtanzania ambao ni Fedilis Felix ambaye amepewa mataba nono wa kupiga picha kwenye Kampuni hiyo.
       Kampuni ya Newhabari ambao inamilikiwa na Bilionea Rostam Azizi pia ilizidi kulibomoa Gazeti la Mwananchi baada ya kuendelea kuwachukua watu wake muhimu ambaye mwengine ni Msambazaji Msaidizi Erasto Matasia.
         Kukimbia huko kwa mwananchi kunatafsiriwa tofauti na wachambuzi wa masula ya Habari kwamba Gazeti hilo linapitia katika kipindi kigumu na linaitaji busara  tu  katika kukabiliana na hali hiyo.
        Akilizungumzia hali hiyo ndani ya Gazeti la mwananchi Msomi  na mchambuzi wa Masuala ya Habari kutoka chuo Kikuu Huria cha Tanzania Bilal soud alisema kwa sasa gazeti hilo limekumbana pigo kubwa sana na dalili zimeonekana baada ya maudhui ya Gazeti hilo kuwa tofauti na kipindi cha nyuma.

“Kusema ukweli bila hata kuuliza kama Meena yupo au Tido utajua tu watu hawa hawapo kwasababu Habari wanazozichapisha sahivi zimekuwa na zikionyesha kwamba gazeti limekosa watu makini kama wakina Tido na wasipotafuta ufumbuzi wanaweza wakawa sehemu sio nzuri”alisema Bilal

No comments