Zinazobamba

EXCLUSIVE--SAMWEL SITTA AZIDI KUWAPUUZA MAASKOFU,AJIFANYA JEURI,SOMA HAPA KUJUA ZAIDI

Na Karoli Vinsent
        KILE kinachoonekana ni kuchoka kisiasa pia kuzeeka, kwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba,Samwel Sitta baada ya hivi sasa kuwapuuza viongozi mbalimbali wa Dini waliomtaka kuacha kuzika maoni ya wananchi yalitolewa kwenye Rasimu ya pili ya Katiba,Mtandao huu unaripoti.
           Viongozi hao wa dini ya Kikristo katika tamko lao walilitoa linasema Bunge maalum la katiba haliwezi kuleta katiba Mpya badala yake litaishia kukwamisha matarajio ya wanananchi ya upatikanaji wa Katiba.
        Tamko hilo la Madhehebu hayo limetolewa na Fungamano la Majukwaa Manne ambayo ni Christian Council of Tanzania (CCT),Tanzania Episcopal Conference (TEC) The Council of Pentecostal Churches of Tanzania (CCPCT) na The Seventh day Adventist,Tamko hilo lilisema wazi kwamba Bunge la katiba alijadili Rasimu ya Katiba bali wanajadili Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM,
         Sitta ambaye ni Waziri wa Uhusiano wa Afrika Mashariki, mara kwa mara amekuwa akiwabeza watu waliokuwa wakimshauri kuhusu kulisitisha Bunge hilo ili kutafuta maridhiano ya Kisiasa lakini bado mwenyekiti huyo anawaita watu hao ni Mbumbu wa hoja.
         Machozi ya Viongozi hawa wa Dini yamekwenda moja kwa moja, kwa mwenyekiti wa Bunge la katiba huyo na kusema Sitta ameshindwa kusimamia Sheria ya iliyotungwa na Wajumbe wake na kwa kitendo chake cha kusema Bunge hilo kwa kisingizio cha wajumbe wengi.
           Tamko hilo la Maaskofu limeibua hoja baada kugundulika kwamba Sitta amevunja Katiba sura ya 83 sheria ya Mabadiliko ya katiba kwa kuzidi kupokea maoni ya wananchi ambapo sheria hiyo imekataza.
         Lakini bado Mwenyekiti huyo anatumia udikteta wake kupinga hoja za Viongozi wa dini hao wanaomtaka asikilize maoni ya wananchi,
        Sitta anazidi kuonekana kukosa usawa wa Kisiasa baada ya Wiki iliyopita Bungeni alimbeza Mwandishi wa Habari Mwandamizi na Mzalendo wa Nchi yake Saed Kubenea ambaye alikwenda kufungua kesi mahakamani kushinikiza Bunge lisitishwa kwa madai halina uharali wa kisiasa,
         Na kuzidi kusema  mwandishi huyo anatumiwa,na kuzidi kujisifia kwamba yeye ni mtu makini na asiyeyumbishwa na mtu na kusema yeye anasifa za kugombani Urais ndani ya chama cha mapinduzi,
           Akilizungumzia hili,Mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi NEC kutoka kwenye mikoa ya kusini ambaye akutaka Jina lake litajwe kwenye Mtandao huu alisema anamshangaa sana Samwel Sitta kwa kuchakaa kwake kimawazo kwa kitendo chake cha kupuuza mawazo ya Viongozi wa Dini.
“Hiki ni kichekesho sana ndugu yangu tena aingii akilini kabisa anachokifanya huyo mzee sitta ni upuuzi kabisa leo ameanza kupokea maoni mapya wakati kazi hiyo ilifanywa na tume ya Jaji warioba,sasa yeye naye anapokea maoni harafu chama kinamwacha wala akimkemei tena,
“ kinamwacha sasa huyo mtu ataleta machafuko tu akiaachiwa hivi na kama anajidanganya atapewa Urais hana sifa hata ya kupewa tena hata ubunge aliokuwa nao”alisema Mjumbe huyo
Rasimu hiyo inayochkachuliwa na Sitta iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba, inapendekeza muundo wa muungano wa Shirikisho la Serikali tatu, lakini CCM imeipindua na kurejesha muundo wa sasa wa Serikali mbili, licha ya kwamba Bunge hilo bado halijafanya uamuzi wa kura kwa sura ya kwanza na ya sita zinazohusu muundo wa muungano.
          Katika taarifa hizo ambazo zinaendelea kuwasilishwa na wenyeviti wa Kamati za Bunge hilo, maoni ya wajumbe walio wengi yamefuta ibara nyingi za mapendekezo ya rasimu na kuingiza mpya, kurekebisha zingine na kuingiza Sura mpya kuhusu masuala kadhaa ambayo Tume ya Jaji Warioba iliyaacha yashugulikiwe na serikali za nchi washirika za Tanganyika na Zanzibar.

                   Sura mpya zilizoingizwa ni kuhusu Ardhi, Rasilimali na Mazingira, Serikali za Mitaa wakati suala la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kamati zimetofautiana kwa wajumbe wengine kutaka iingizwe katika Sura ya kumi na tatu ya rasimu inayohusu Taasisi za Uwajibikaji

No comments