Zinazobamba

MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE---SERIKALI YA TANZANIA INATAFUTA KINGA YA KUWAKINGA WANAOFANYA MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE.SOMA HAPA UJUE KWANINI



Pichani ni Mwenyekiti Mtendaji  wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania TACAIDS Dkt Fatma Mrisho picha na Maktba
Na Karoli Vinsent

SERIKALI Imesema iko mbioni kutafuta  njia itakayoweza  kuwasaidia watu wanaofanya mapenzi ya kinyume na maumbile ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali.
            Kauli hiyo  imetolewa leo Jijini Dar es Salaam, na Mganga mkuu wa Serikali Dkt.Donnan Mbando wakati wa mkutano na waandishi wa Habari katika mkutano huo uliandaliwa mahususi kwa ajili ya kuzungumzia kuhusu mkutano wa 20 wa Kimataifa wa Ukumwi Duniani uliofanyika mwezi wa saba mwaka huu nchini Melbourne nchini Austaria.
           Ambapo alisema kwa sasa serikali ya Tanzania iko mbioni kutafuta njia ya kuwasaidia watu wanaofanya mapenzi kinyume na maumbile ili wasiweze kupata magonjwa.

      “Na sasa  serikali inatafuta njia ya kuweza kuwakinga watu wanaofanya Mapenzi kinyume na maumbile ili waweze kujikinga na magonjwa kwani tumegundua katika mkutano huo kwamba sababu inayopelekea maambukizo ya ukimwi yanatokana na watu kufanya mapenzi kinyume na maumbile sasa  imekuwa ni kubwa,na sasa tumegundua watu hao hawezi kuacha “alisema Mbando.
             Kwa upande wake Mwenyekiti Mtendaji  wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania TACAIDS Dkt Fatma Mrisho alisema wao wamejipanga kuwapa elimu Madaktari na wahudumu wengine wa afya iliwaweze kuwapa huduma za Afya bila ya kuwatenga watu wanaofanya mapenzi kinyume na Maumbile.
           “Mwaka jana katika Ripoti ya Haki za Binadamu ilikuwa inasema Tanzania inawanyapaa watu wanaofanya mapenzi ya Jinsia moja,nataka              niwambie sio kweli Tanzania haiwatengi watu wanaofanya mapenzi ya jinsia Moja ambapo sio kweli kabisa,na sasa tume yangu iko mbioni kuwapa elimu wa wahudumu wa Afya wasiwanyapae watu hawa”alisema Dkt Mrisho.  

No comments