Zinazobamba

MAMALAKA YA ELIMU TEA YAUNGANISHA NGUVU NA WADAU KUSAIDIA KUONDOA TATIZO LA WANAFUNZI KUKETI CHINI, 156000000 ZATUMIKA KUNUNUA MADAWATI,

IMG_8357Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano toka Mamlaka ya Elimu Tanzania Bi Sylvia Lupembe akiongea na waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu jitihada wanazofanya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kukabiliana na changamoto katika sekta ya elimu,wakati wa mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na Uhusiano toka benki ya KCB Bi. Christina Manyenye. IMG_8369Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo wakiwasikiliza wawasilishaji toka Mamlaka ya Elimu Tanzania, KCB, TOTAL, Social Action Trust Fund (SATF) leo Jijini Dar es Salaam.
IMG_8380Mkuu wa kitengo cha Masoko na Uhusiano toka benki ya KCB Bi. Christina Manyenye akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) mipango waliyoiweka kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu Tanzania katika kuendeleza na kuinua sekta ya Nchini.kushoto ni Meneja Sheria na Uhusiano toka kampuni ya uuzaji na usambazaji wa mafuta ya TOTAL Bi. Masha Msuya. 
IMG_8401Afisa Rasilimali Fedha toka taasisi isiyo ya kiserikali ya Social Action Trust Fund (SATF) Bw. Timotheo Tenga akiwaeleza jambo waandishi wa habari( hawapo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Sheria na Uhusiano toka kampuni ya uuzaji na usambazaji wa mafuta ya TOTAL Bi. Masha Msuya
Daresalaam,
Mamlaka ya elimu TEA kwa kushirikiana na makampuni ya ndani ya nchi wametoa msaada wa madawati 2000 kwa shule 10 za jijini Darsalaam ikiwa ni jitihada za kuondoa changamoto zinazowakabili wanafunzi wanaosoma katika mazingira magumu
Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo, meneja habari ,Elimu na mawasiliano wa mamlaka hiyo B. Silyvia Lupembe amesema msaada huo unatarajiwa kunufaisha jumla ya wanafunzi 6000 katika shule 10 huku jitihada zingine zikichukuliwa kuwafikia wanafunzi wengine wanaosoma wakiwa wamekaa chini nje ya jiji la Daresaalam
Bi Lupembe alizitaja shule ambazo zinatarajiwa kunufaika na udhamini huo wa madawati kuwa ni pamoja na shule ya msingi Chamazi,Mbande,,Boko,,NHC,Hekima,Bwawani,Bunju, na Kingugi, Zingine ni shule ya msingi Kombo,Goba,na King’ong’o
Bi Lupembe ametoa wito kwa makampunii mengine yenye nia ya kusaidia katika sekta ya elimu kujitokeza na kuja kusaidia watoto wetu ambao wanasoma katika mazingira magumu ambayo hayamruhusu kupata elimu iliyo bora kutokana na miundo mbinu ya shule kutoruhusu kutoa elimu iliyo bora
Naye afisa mahusiano wa kampuni ya mafuta ya TOTOL ambao wameanzisha mchakato huo wa kufadhili madawati kwa shule zenye uhitaji mkubwa, Bi Masha Kileo amesema wazo la kuja kusaidia shule zilizo katika uhitaji mkubwa wa madawati limekuja baada ya kuona wanafunzi wakisoma katika mazingira mabovu huko shule za msingi,
Bi Kileo ameongeza kusema kuwa madawati hayo ambayo yanatarajiwa kukabidhiwa kwake katika shule hizo za jijini Daresalaam yameghalimu jumla  ya shilingi million 156,000,000 ambazo zimechangiwa kwa pamoja na kampuni ya KCB bank, na mfuko wa kusaidia jamii wa Social Action Trust Fund (SATF).
MAGARI…………………….PRESS…………………21.08.2014

No comments